logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanafunzi wa Darasa la 6 aua mwanafunzi mwenzake kwa ajili ya ugali huko Kakamega

Wanafunzi hao wawili walikuwa majirani.

image
na Radio Jambo

Habari15 October 2021 - 10:04

Muhtasari


  • Polisi katika Kaunti ya Kakamega wanamshikilia mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 14 anayedaiwa kumuua mwenzake kwa ajili ya Ugali na Kunde

Polisi katika Kaunti ya Kakamega wanamshikilia mwanafunzi wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 14 anayedaiwa kumuua mwenzake kwa ajili ya Ugali na Kunde.

Mwanafunzi huyo anaripotiwa kuutupa mwili wa marehemu katika Mto Simakina huko Navakholo, Kaunti ya Kakamega.

OCPD wa Navakholo Richard Omanga alithibitisha kisa hicho akisema, marehemu mwenye umri wa miaka 10 alikuwa akichunga ng'ombe wa familia yake wakati alipovamiwa na kushambuliwa na mwanafunzi mwenzake.

Wanafunzi hao wawili walikuwa majirani.

Inaripotiwa kuwa mwanafunzi huyo wa Darasa la Sita alifika nyumbani kutoka shuleni Alhamisi na akaarifiwa kuwa chakula alichokusudia kula kilikuwa kimeliwa na jirani yake.

Kisha alimfuata na kumpiga kichwani na kifaha butu, na kumuua papo hapo kabla ya kutupa mwili wake mtoni.

Siku ya Ijumaa, mtoto huyo alifika shuleni na kuwaarifu walimu wake kwamba alikuwa amemuua mwenzake 

OCPD pia alisema kwamba kichwa cha marehemu kilikuwa na majeraha ya kichwa, na mwili wake umepelekwa katika makafani ya kuhifadhi maiti ya hopsitali ya rufaa ya Kakamega.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved