logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke afariki baada ya kupatikana chumba kimoja cha kulala Mtito Andei

Mwanamke afariki baada ya kupatikana chumba kimoja cha kulala Mtito Andei

image
na

Habari02 October 2020 - 12:49
Kifo
Mwanamke 25, afia daguroni Mtito Andei.

Maafisa wa polisi huko Mtito Andei kaunti ya Makueni wameanzisha uchunguzi baada ya mwanamke mwenye umri wa miaka 25 kupatikana amefariki kwenye chumba kimoja cha kulala mjini humo.

Kulingana na naibu OCPD wa Kibwezi Geoffrey Nderitu, mwili wa mwendazake ulipatikana na wafanyikazi wa eneo hilo la burudani walipokuwa wakifanya usafi.

Nderitu anasema bado haijabainika iwapo mwanamke huyo alikuwa na mpenziwe alipokodi chumba katika eneo hilo linalotumiwa sana wafanyibiashara wa ngono.

Mwili wake umehifadhiwa katika hifadhi ya  maiti ya Makindu huku uchunguzi ukianza.

-Solomon Muingi.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved