Kilichomfanya kujitokeza na kuongea ni kwa sababu alikuwa ametolewa kutoka kwa mambo hayo maovu na mhubiri mashuhuri T. B Joshua.
Baada ya kupeleka onyo kwenye mtandao wa Facebook, mwanamke huyo aliendelea kuelezea jinsi wanavyotumia vyombo vya habari vya kijamii ili kukuvutia watu
katika mambo hayo alielezea na kusema,
"Mimi nina umri wa miaka 42 lakini ninaye mjukuu. Nilianzishwa katika kikundi hiki nilipokuwa na umri wa miaka 25.
Niliitoa nafsi ya mtoto wangu ambaye alikuwa na miezi 9 kwa wakati huo.
Baada ya wiki moja nilianza kuzipata hela amabazo sikujua zilipotoka na kufungua biashara ya viatu ambapo viatu hivyo vya Gikomba vilinipa 400k kwa mwezi.
Nilipata maagizo kutoka mbali kama Lebanon, Marekani, Australia na Dubai, watu walitaka kuvinunua viatu vile.
Nilikuwa nikiishi Kawangware lakini baada ya mwezi mmoja nilihamia Kileleshwa, nikanunua gari, na ardhi na kufungua maduka mawili mjini na Mombasa.