logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO: Ndugu yangu alitumia simu ya mzee kufuliza

PATANISHO: Ndugu yangu alitumia simu ya mzee kufuliza

image
na

Burudani02 October 2020 - 02:49
Kevin alituma ujumbe akiomba apatanishwe na nduguye bwana George.

Alisimulia,

"Tulikosana na ndugu yangu Mei mwaka huu kwani kulikuwa na shida nyumbani baada ya mzee kuniambia kuwa hawana pesa za chakula. Nilikuwa na elfu moja ambayo nilipea wife akasongwe nywele, kumwambia mke wangu akasema atatuma mia tano.

Sasa mzee hana uwezo wa kutumia Mpesa na lazima mtu amsaidie. Mhudumu wa Mpesa alimwambia hana fedha na kuthibitisha ni kuwa Fuliza ilikuwa imekataa zile fedha.

Kevin anasema alipomuuliza ndugu mdogo alisema sio yeye aliyefuliza kwani hakuwa nyumbani kwa mwezi mmoja. Mhudumu wa Mpesa akasema kuwa nduguye mkuu ndiye aliyefuliza.

Alipompigia simu nduguye mkuu walikosana kwani tayari alijua mbona anapigiwa na isitoshe haikuwa mara ya kwanza.

Hata hivyo, juhudi zetu za kumfikia George hazikufua dafu kwani tayari alikuwa amezima simu yake huku Kevin akisema kuwa yeye alisema kama anataka msamaha basi anapaswa kwenda nyumbani.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved