Lady Maureen yuko katika hospitali ya Jaramogi Oginga ambapo amelazwa hapo kwa muda.
"Support a woman and save the village. We are doing this as #teamakothee. Action is better than a pity party." Akothee Alisema.
Alisema kuwa hakuweza kumpa shamba la kuishi kwa maana hakuna mtu yeyote wakumsaidia kwa hivyo alikuwa mikononi sawa ya familia yake, na hawakuwa na ukoo wowote.
""She is safe with her relatives." Alisema Akothee.
Maureen ambaye alitoka hospitali tarehe 20,Februari hakuwa na mahali pa kuenda kwa maana familia yake ilimkataa, lakini Mungu hamwachi mja wake Msamaria mwema Nancy Achieng alimchukuwa na kuanza kumsaidia kwa vyovyote vile.
Akiwa katika mahojiano Nancy alisema,
" Niliongea na mama yake na akaniambia nisimpeleke nyumbani kwake." Alieleza.
Akothee amesema kuwa mjomba wake amempa shamba baada ya familia yake kumkataa.
"Niliwasiliana na mmoja wa wajomba wake na lady Maureen yupo katika nyumbani mwake, amejitolea kumpa shamba ambayo anapaswa kujenga nyumba yakeMama yangu ataenda Nyakach kwa niaba yetu." Akothee Aliandika katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram.
Mama Maureen alipokuwa katika mahojiano alisema kuwa rafiki zake Maureen walimtenga baada ya kulazwa hospitali.
"Wale wote walikuwa wanakula blueband na Maureen Nairobi wote walimtoroka." Alizungumza mamake Maureen.
Akufahaye kwa dhiki ndiye rafiki na pia hawakukosea walipo sema rafiki ni kufahana wala si kufanana.
