logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Washukiwa 10 watoroka kutoka kituo cha polisi cha Bungoma

Washukiwa 10 watoroka kutoka kituo cha polisi cha Bungoma

image
na

Burudani01 October 2020 - 10:14

Polisi katika kaunti ya Bungoma wameanzisha msako wa majangili 10 ambao walitoroka kutoka kituo Kikuu cha Polisi cha Bungoma.

Polisi wanasema kundi hilo lilitoroka mwendo wa saa tisa asubuhi hii leo baada ya kuchimba shimo ukutani wakati wa usiku.

Maafisa wa usalama walifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja ambaye alipigwa risasi kwenye paja alipokuwa akijaribu kutoroka.

Hayo yakijiri wizara ya masuala ya ndani hapo kesho itazindua kampeni ya usafishaji wa vituo vyote vya polisi na magereza, huku zoezi hilo likianzishwa katika kaunti ya Nairobi. Waziri Fred Matiang'i anasema hii ni sehemu ya mradi wa serikali unaoendelea unaonuwia kuboresha utoaji huduma kwa wakenya.

Kwingineko, wakaazi wa jiji la Nairobi kuanzia kesho wataweza kupata huduma za serikali katika kituo cha Huduma Center cha GPO baada ya kituo hicho kufungwa yapata mwezi mmoja sasa ii kufukizwa dawa kutokana na ongezeko la visa vya Corona jijini. Hata hivyo ili kupunguza msongamano na muda unautumia ukipanga foleni, utahitajika kupanga miadi kwanza. Ili kupanga miadi, tembelea tovuti www.hudumakenya.go.ke, bonyeza weka miadi au book appointment kisha fuata hatua za jinsi ya kuweka miadi ya huduma inayotaka.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved