logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Idadi ya waliofariki kwa ajili ya Covid 19 yafika 664 baada ya watu 5 zaidi kufariki

Idadi ya waliofariki kwa ajili ya Covid 19 yafika 664 baada ya watu 5 zaidi kufariki

image
na

Yanayojiri01 October 2020 - 09:20
Visa vipya 130 vya covid 19 vimeripotiw anchini na kufikisha jumla ya visa hivyo kuwa  37,348 ,  amethibitisha waziri wa Afya Mutahi Kagwe .

Visa hivyo ni kutoka sampuli 3,874 zilizopimwa katika kipindi cha saa 24 zilizopita  na kufikisha jumla ya sampuli zilizopimwa hadi sasa kuwa 523 .998 .

Kiwango cha maambukizi sasa kipo asilimia 3.34.

Visa vyote ni vya  wakenya isipokuwa  saba ambao ni raia wa kigeni .

Watu watano Zaidi wameaga dunia na kufikisha idadi ya walioangamizwa na ugonjwa huo nchini kuwa 664 .

Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema mgonjwa wa umri wa chini ana miaka mitatu ilhali wa umri wa juu ana miaka 90 .

Nairobi inazidi kuongoza kwa visa vingi baada ya visa 35 kusajiliwa katika saa 24 zilizopita Kiambu (23), Kisumu (19), Mombasa (14), Uasin Gishu (8), Kerich (6), Kisii (5), Busia (5), Kilifi (5), Bomet (2), Narok (2), Siaya, Trans Nzoia, Turkana, Kajiado  na  Machakos  zikiwa na kisa 1 kila moja

Watu wengine 106 wamepona na kufikisha idadi ya waliopona ugonjwa huo nchini kuwa  24 ,253 .

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved