logo

NOW ON AIR

Listen in Live

3 watekwa nyara na wanamgambo wa Al Shabaab Mandera

3 watekwa nyara na wanamgambo wa Al Shabaab Mandera

image
na

Burudani01 October 2020 - 09:19
Watu watatu hawajulikani waliko baada ya kutekwa nyara na washukiwa kundi la kigaidi la Al Shabaab katika kaunti ya Mandera siku ya Jumatano jioni.

Polisi wanasema kwamba wahasiriwa ni mafundi na walikuwa safarini kuelekea eneo la Lafey kufanya kazi.

Kisa hicho kilitokea umbali wa kilomita 30 kutoka mji wa Lafey wakati gari la usafiri wa umma ambamo watatu hao walikuwa wakisafiria lilisimamishwa na watu waliokuwa wamejihami kwa silaha kali.

Watatu hao ambao si wenyeji walikuwa wageni katika eneo hilo na kwa sasa haijulikani waliko.

Vikosi vya usalama vimeanzisha oparesheni ya kuwasaka huku hali wasi wasi ikitanda kwa hofu kuwa huenda wanamgambo wa Al Shabaab wako katika eneo hilo.

Kuna hofu pia kwamba huenda kisa hicho kimechangiwa na malumbano ya kisiasa katika eneo hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved