logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ghost Mulee ahusika katika ajali ya barabarani

Mulee alikimbizwa hospitalini punde tu baada ya ajali na yuko katika hali thabiti.

image
na Radio Jambo

Burudani16 October 2020 - 05:56

Muhtasari


• Alikuwa njiani akielekea kazini mwendo wa saa kumi na moja asubuhi

• Alikimbizwa hospitalini na hali yake ni thabiti 

• Gari lake liligongwa na matatu katika upande wa dereva 

Gari la Ghost Mulei punde tu baada ya ajali siku ya Ijumaa

Mtangazaji wa Radio Jambo Jacob Ghost Mulee amehusika katika ajali ya barabarani mapema siku ya Ijumaa alipokuwa anaelekea kazini.

Mulee alikimbizwa katika hospitali ya Agha Khan punde tu baada ya ajali hiyo kutokea na yuko katika hali thabiti.

Gari la mtangazaji huyo wa kipindi cha ‘Gidi na Ghost asubuhi' liligongwa kwa upande wa dereva na matatu mwendo wa saa saa kumi na moja unusu.

Ghost Mulee
 
 
 
 

Ajali hiyo ilitokea katika eneo la Brookside kwenye barabara kuu ya Waiyaki, wakati gari lake lilipogongwa  na matatu ya KMO iliyokuwa ikiendeshwa kwa kasi kuelekea mjini Nairobi kutoka eneo la Kangemi.

Gari la Ghost ambalo limeharibika vibaya limevutwa hadi kituo cha polisi cha Spring Valley.

Alikimbizwa hospitalini na msanii Jalang'o ambaye amesema alikuwa anafanyiwa vipimo kuthibitisha ikiwa alipata majeraha zaidi.

Meza ya habari ya Radio Jambo inamuombea Ghost afueni ya haraka.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved