logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fuatilieni shughuli za watoto wenu wakiwa nyumbani na mitandaoni ,DCI yaonya

Mkuu Wa DCI  George Kinoti  amesema wanalisaka genge la wahalifu ambalo linawatumia watoto kufanya vitendo visivyo halali

image
na Radio Jambo

Burudani21 November 2020 - 12:40

Muhtasari


  •  Mkuu Wa DCI  George Kinoti  amesema wanalisaka genge la wahalifu ambalo linawatumia watoto kufanya vitendo visivyo halali
  •  DCI  imewaokoa wasichana sita walioripotiwa kupotea  baada ya video kusambazwa mitandaoni kutaka maelezo yatakayosaidia warejee nyumbani

 

 Idara ya DCI imewashauri wazazi  kuwa waangalifu kuhusu mienendo ya watoto wao wakiwa nyumbani na wanachofanya mitandaoni

 Mkuu Wa DCI  George Kinoti  amesema wanalisaka genge la wahalifu ambalo linawatumia watoto kufanya vitendo visivyo halali

Kinoti  amewaonya wazazi kwamba wanafaa kufuatilia shughuli za wanao mitandaoni pia

" Uchunguzi ukiendelea tungependa pia kuwaonya watu wanaowatumia watoto kutekeleza uhalifu na kujihusisha na vitendo vingine vibaya kupitia mitandao ya kijamii’ amesema Kinoti

 Makachero wanalichunguza kundi moja linalotumia mitandao ya kijamii kuwatumia waichana wa shule kujihusisha na  uhalifu kama vile kuteneza picha za  ponografia na kuwafanya watoto hao kutoweka kutoka majumbani kwa siku kadhaa .

 DCI  imewaokoa wasichana sita walioripotiwa kupotea  baada ya video kusambazwa mitandaoni kutaka maelezo yatakayosaidia warejee nyumbani .

 Kulingana na mwanamke mmoja aliyetengeza ombi hilo kupitia njia ya video  wasichanahao walitoweka tarehe 14 Novemba  baada ya kuhadiwa kutoka makwao na mtu aliyejulikana  .wasichana hao saba walikuwa na umri wa miaka 16 kutoka mtaa wa Komarock ,Nairobi

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved