logo

NOW ON AIR

Listen in Live

PATANISHO: Mume wangu aliniletea nguo akiwa amepaguzia uchafu wa mwanamke

"Tumekuwa kwa ndoa kwa miaka kumi na nne, mume wengu ni makanga

image
na Radio Jambo

Burudani26 November 2020 - 06:12

Muhtasari


  • mume wangu amekuwa akinitesa sana naomba mnipatanishe ili abadilike
  • Juzi aliniletea shati likiwa na uchafu wa mwanamke
  • Shati hilo haikuwa na uchafu wa mwanamke ilikuwa dawa ya meno

Leo katika kitengo cha patanisho Bi Linet alituma ujumbe ili apatanishwe na mumewe ambaye wamekuwa wakikosana kwa muda.

"Tumekuwa kwa ndoa kwa miaka kumi na nne, mume wengu ni makanga amekuwa akirudi nyumbani akiwa amelewa chakari, hivi juzi aliniletea shati lake likiwa na uchafu wa mwanamke ili nioshe

Nikimuuliza anapinga kila kitu nikimpelekea kwa wazazi ili wazungumze naye ili abadilike baba yake anakuwa uoande wake wanaanza kubugia vileo pamoja." Alieleza Linet.

Kwa upande wake bwana Timothy alikuwa na haya ya kueleza;

"Mimi nilimuoa huyu mwanamke nimekuwa nikifanya kazi kwa bidii ili kupata riziki ya kila siku, amekuwa akisikiza manaeno ya watu wengine, hakuna siku ambayo nimelala nje shati ambalo anasema nilipiga mswaki nayo na nikajipangusia dawa huo haukuwa uchafu wa mwanamke

Hii kazi yetu huwa tunafunga usiku nikimaliza naenda nyumbani nafika napata mama amekasirika vibaya." Alisema Timothy.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved