Mwanahabari,muigizaji Joey Muthengi alifahamika sana wakati alionekana na kuwa mmoja wa wasimamizi wa kipindi cha Tusker Project Fame SS6 wakati mwaka wa 2014.
Joey alisema kwamba wakati huo alikuwa ametoka mbali kutoka kwa kusongwa na mawazo akiwa na umri wa chini hadi kuachwa na mpenzi wake.
"Baada ya kuonekana katika kipindi cha Tusker Project Fame,nilikejeliwa sana kwenye mitandao ya kijamii
Nilienda kulia kwa mudaa wa saa moja, kutoka hapo niliamua kurudi tena hata baada ya kukejeliwa kwa muda wa miezi sita, kwa sababu niliangalia mahali nimetoka ni mbali sana
Niliamua kukaa mbali na mitandao ya kijamii kwa muda." Aliongea Muthengi.
Muthengi alisema baada a kukejeliwa aliongea na watu tofauti ikiwemo ndugu yake na kumwambia kuwa asijali kwa maana anaweza kazi hiyo.
Pia alidai kwamba watu katika kipindi hicho walikuwa wamempenda.
