logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Anne Kananu achukuwa wadhifa wa kaimu gavana wa Nairobi

Anne Kananu achukuwa wadhifa wa kaimu gavana wa Nairobi

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 January 2021 - 09:45

Muhtasari


  • Ann Kananu siku ya Jumatatu alichukuwa usukani kuongoza kaunti ya Nairobi kama kaimu Gavana.

  • Kananu ataendelea kushikilia nafasi yake kama naibu gavana akisubiri uthibitisho kama Gavana.

Naibu gavana Anne Kananu apokea zana za kuhudumu kama kaimu gavana wa Nairobi kutoka kwa Benson Mutura

Ann Kananu siku ya Jumatatu alichukuwa usukani kuongoza kaunti ya Nairobi kama kaimu Gavana wa kaunti hiyo siku tatu tu baada ya kuapishwa kuwa naibu gavana. 

Spika wa Bunge la Kaunti ya Nairobi Benson Mutura Jumatatu alimkabidhi Kananu rasmi zana za mamlaka katika hafla iliyoandaliwa katika makau makuu ya jiji la Nairobi City Hall.

Mutura alisema kwa sababu Nairobi sasa ina Naibu Gavana hana budi kuachilia mamlaka kama Kaimu Gavana na kurejelea majukumu yake kamili kama Spika.

"Mimi sio mwanasiasa, na sitaanza kuwa mmoja. Ninalenga kuleta azma mpya ya ushirikiano, ushirikiano na  kuheshimiana na idara zote za serikali. Nairobi sasa imerejea kwa mkondo wa maendeleo," Kananu alisema.

Kananu ataendelea kushikilia nafasi yake kama naibu gavana akisubiri uthibitisho kama Gavana wakati kamati ya ukabidhi wa mamlaka itakapokamilisha mchakato wa ubadilishanaji mamlaka.

Ijumaa iliyopita, Kamati ya Uteuzi iliyoongozwa na Kiongozi wa Wengi Abdi Guyo ilimpiga msasa na kumuidhinisha Kananu kuhudumu kama naibu gavana.

Katika hotuba yake ya kwanza kama naibu gavana, Kananu alisema atafanya kazi bila kuchoka pamoja na mkurugenzi mkuu wa Huduma ya Metropolitan ya Nairobi Meja Jenerali Mohammed Badi kuhakikisha kazi zote zilizohamishwa zinaimarishwa zaidi kuhakikisha huduma zinatolewa kwa wakaazi wa Nairobi.

Kananu pia aliahidi kuunda kamati ya uhusiano kati ya kaunti na NMS ili kuimarisha tendakazi wa jiji la Nairobi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved