logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hayati John Pombe Magufuli kuzikwa hii leo Chato Tanzania

Hayati John Pombe Magufuli kuzikwa hii leo Chato Tanzania

image
na Radio Jambo

Burudani26 March 2021 - 05:24

Muhtasari


• Maelfu ya wananchi tayari wameanza kujitokeza katika uwanja wa Magufuli ambapo kutakuwa na misa maalumu ya wafu kuombea nafsi ya mwendazake.

• Kabla mazishi mwili wa Magufuli utapelekwa katika kanisani kwa ibada maalumu.

Marehemu rais John Pombe Magufuli

Hayati John Pombe Magufuli ambaye kufikia kifo chake alikuwa rais wa Tanzania anazikwa leo nyumbani kwake eneo la Chato katika makaburi ya familia.

Maelfu ya wananchi tayari wameanza kujitokeza katika uwanja wa Magufuli ambapo kutakuwa na misa maalumu ya wafu kuombea nafsi ya mwendazake.

Kabla mazishi mwili wa Magufuli utapelekwa katika kanisani kwa ibada maalumu.

Rais Magufuli alifariki kutokana na maradhi ya moyo wakati alipokuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam tarehe 17 Machi.

Magufuli ni rais wa kwanza nchini Tanzania kufariki akiwa madarakani na hatua hiyo inalifanya taifa hilo kuongozwa na rais mwanamke kwa mara ya kwanza, Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa siku kadhaa sasa, baadhi ya wakazi wa mji wa Chato na viunga vyake waliokuja kuaga mwili wa rais John Pombe Magufuli. wamelazimika kulala katika mazingira magumu huku wakipigwa na baridi ya usiku kutoka Ziwa Victoria.

Rais Magufuli atakumbukwa kwa kuanzisha miradi kadhaa ya maendeleo nchini Tanzania.

Marehemu kiongozi huyo hata hivyo alijipata katika njia panda na viongozi wengine wa kanda Afrika Mashariki kutokana na vile alikuwa akishughulikia janga la Covid-19.

Chini ya uongozi wake serikali ya Tanzania ilidinda kutoa takwimu za maambukizi.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved