logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamuziki wa Gengetone atafuta haki ya mwanawe aliyeaga katika harakati ya kuzaliwa

Lexy Yung wa kikundi cha sailors analaumu muuguzi katika hospitali ya Limuru kwa kumdunga mwanawe akiwa bado  tumboni mwa mpenzi wake

image
na Radio Jambo

Burudani08 June 2021 - 06:38

Muhtasari


•Yung amelaumu muuguzi huyo kwa kumpokonya mwanawe ambaye alikuwa amesubiria kwa hamu sana. huku akiapa kuwa ni sharti atafute haki ya mwanawe

•Mpenzi wa Yung, Muthoni almaarufu kama @sexy_wa_lexxy, amesema kuwa amekubali mwanawe kupumzika kwa amani huku akisema kuwa ilikuwa kazi ya Mungu na haiwezi kosolewa.

Lexy Yung na Mpenzi wake Faith Muthoni

Mmoja wa wasanii kwenye  kikundi cha Sailors Gang, Lexy Yung pamoja na mpenzi wake Faith Muthoni wanaomboleza kupoteza kitinda mimba chao wakati alikuwa anazaliwa.

Lexy Yung

Kupitia ukurasa wa Instagram, yung amesema kuwa wawili hao walikuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza usiku wa Ijumaa baada ya Muthoni kupata uchungu wa uzazi na kulazwa katika hospitali ya Limuru.

Mwanamuziki huyo wa nyimbo aina ya gengetone analaumu hospitali ya Limuru kwa kile alichosema ni utepetevu wa mkunga aliyekuwa anasaidia mpenziwe kuzaa.

"Ni msumari uliodungwa kwenye moyo wangu na wa mke wangu.. Tumekuwa na raha tele na tumejitayarisha kumpokea kitinda mimba wetu. Siku hiyo hatimaye ilifika, Juni 4 na ambapo tulipata uchungu wa uzazi mida ya usikuna tukaenda katika hospitali ya Limuru almaarufu kama Patel. Bibi yangu alilazwa na nikaagizwa niende nyumbani nirudi asubuhi ifuatayo. Siku iliyofuata nilirejea hospitali nikiwa nimejawa na raha tele ila habari za kuhofisha zilikuwa zimenisubiria. Muuguzi alipasua maji ya bibi (sijui kama yafaa kupasuliwa) na katika harakati hiyo akadunga mtoto wangu aliyekuwa mzima" Yung aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Msanii huyo amesema kuwa alielezwa na daktari kuwa mtoto wake alikuwa amedungwa katika harakati ya muuguzi kupasua maji ya mkewe.

Yung amelaumu muuguzi huyo kwa kumpokonya mwanawe ambaye alikuwa amesubiria kwa hamu sana. huku akiapa kuwa ni sharti atafute haki ya mwanawe.

Kwa upande wake Muthoni almaarufu kama @sexy_wa_lexxy amesema kuwa amekubali mwanawe kupumzika kwa amani huku akisema kuwa ilikuwa kazi ya Mungu na haiwezi kosolewa.

"Mungu anapeana na anachukua pia kwani anajua mipango aliyo nayo kwetu . Namuachia kila kitu kwani siwezi beba uchungu huo tena. Nashukuru mpenzi wangu Lexy Yung kwa kuwa nami na kuhisi uchungu wangu pia, wewe ni tuzo la maana sana Mungu alilonipa" Faith aliandika kwenye mtandao wa Instagram.

Yung ameeleza kuwa alikuwa amejipanga kabisa kupokea mtoto huyo akisema kuwa alikuwa ashanunua manguo na vitu zingine ambazo mtoto angehitaji ila hakuweza kumsherehekea mwanawe.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved