logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Homabay: Polisi awindwa kwa kudunga sehemu za siri za mkewe baada ya kushuku anamcheza

Alishuku kuwa mkewe alikuwa anatoka nje ya ndoa baada ya kuchukua simu yake na kuangalia watu aliokuwa anazungumza nao

image
na Radio Jambo

Burudani21 June 2021 - 07:02

Muhtasari


•Familia ya mhasiriwa imeeleza kuwa mshukiwa alikuwa amerudi nyumbani kutoka kazini na kuchukua simu ya mkewe ili kuangalia watu ambao alikuwa anawasiliana nao akiwa kazini.

•Babake mhasiriwa, Alfeus Ongou amesema kuwa binti yake alijaribu kueleza bwana yake kuwa walikuwa wakizungumza kuhusiana na masomo ya wanao watatu ila bwanake ambaye ni afisa pande hizo  za Homabay hakutaka kuskia.

crime scene 1

Maafisa wa polisi upande wa Homa Bay wanamtafuta mwenzao anayedaiwa kudhulumu mkewe baada ya kushuku kuwa alikuwa anamcheza na naibu mwalimu mkuu.

Inadaiwa kuwa mshukiwa alitumia kucha zake kudunga sehemu za siri za mkewe wakiwa nyumbani kwao katika kijiji cha maeneo ya Rachuonyo, Homabay.

Familia ya mhasiriwa imeeleza kuwa mshukiwa alikuwa amerudi nyumbani kutoka kazini na kuchukua simu ya mkewe ili kuangalia watu ambao alikuwa anawasiliana nao akiwa kazini.

Hapo ndipo alitilia shaka simu nyingi ambazo mkewe alikuwa anapigiana na mwalimu mmoja kutoka shule moja maeneo hayo ya Rachuonyo.

Babake mhasiriwa, Alfeus Ongou amesema kuwa binti yake alijaribu kueleza bwana yake kuwa walikuwa wakizungumza kuhusiana na masomo ya wanao watatu ila bwanake ambaye ni afisa pande hizo  za Homabay hakutaka kuskia.

Hapo na hapo akaanza kumpiga kabla ya kumdunga kwenye sehemu zake za siri kwa kutumia kucha zake.

"Nahofia kwa kuwa binti yangu amedhulumiwa vibaya. Mpaka alimdunga kwa kucha zake. Nahofia huenda akamuua"  Ongou alisema.

Kesi hiyo iliripotiwa katika kituo cha polisi cha Oyugis usiku huo kabla ya mhasiriwa kuenda kutibiwa katika hospitali ya Rachuonyo.

Naibu Kamishna wa kaunti, David Kiprop amelaani kitendo hicho na kukiita cha kikatili huku akiahidi kuwa mshukiwa atafunguliwa mashtaka punde baada ya kukamatwa. 

Kiprop alisihi walio kwenye ndoa kusuluhisha migogoro yao kwa njia ambayo haisababishi madhara kama vile kuhusisha wazee wa kijiji na wataalam wa kushauriana kuhusu mambo ya ndoa.  


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved