logo

NOW ON AIR

Listen in Live

(+Video) +254 yapatana na Bongo: Mastaa Otile Brown na Darassa watoka jikoni na kibao moto

Wawili hao ambao wana weledi mkubwa wa mistari ya muziki na ufuasi mkubwa kote Afrika Mashariki wameshirikiana kuimba kibao 'K.O(Tiktok)' ambacho kimepakiwa mtandaoni wa YouTube alasiri ya leo.

image
na Radio Jambo

Burudani03 August 2021 - 09:19

Muhtasari


•Baada ya kuwa jikoni kwa muda hatimaye Otile Brown na staa wa Bongo Darassa wametupakulia kibao moto kweli.

•Hapo awali Otile alikuwa amedai kuwa kulikuwa na vikwazo vilivyofanya kibao hicho kisiachiliwe wiki iliyopita ila kwa sasa wimbo huo unapatikana YouTube.

Baada ya kuwa jikoni kwa muda hatimaye Otile Brown na staa wa Bongo Darassa wametupakulia kibao moto kweli.

Wawili hao ambao wana weledi mkubwa wa mistari ya muziki na ufuasi mkubwa kote Afrika Mashariki wameshirikiana kuimba kibao 'K.O(Tiktok)' ambacho kimepakiwa mtandaoni wa YouTube alasiri ya leo.

Wimbo huo ambao ni wa kusifia urembo wa wanadada unaanza na sehemu ya Otile Brown kisha kufunga na sehemu ya Darassa.

Hapo awali Otile alikuwa amedai kuwa kulikuwa na vikwazo vilivyofanya kibao hicho kisiachiliwe wiki iliyopita ila kwa sasa wimbo huo unapatikana YouTube.

"Nafahamu tulistahili kuachia wimbo wiki hii ila kuna mambo hayajakuwa sawa.,. na kwa kuwa wiki tayari imeisha tunaomba tutoe wiki ijayo" Otile alisema Ijumaa wiki iliyopita.

Tazama:-

Je maoni yako ni yepi kuhusiana na kibao 'K.O' wameweza au la??

Wimbo huo umepokewa vyema na mashabiki huku ukiwa umetazamwa na zaidi ya watu 30,000 tangu kuachiliwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved