logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshtuko Nyeri baada ya jamaa kuua ndugu yake mkubwa kwa upanga kufuatia mzozo wa kiti

Maina alikuwa ametumwa na mama yao kuenda kwa ndugu yake mdogo kuchukua sofa ambayo alikuwa amechukua  wakati malumbano makali yaliibuka kati yao na vita ikaanza.

image
na Radio Jambo

Burudani02 September 2021 - 02:30

Muhtasari


• Maina alikuwa ametumwa na mama yao kuenda kwa ndugu yake mdogo kuchukua sofa ambayo alikuwa amechukua  wakati malumbano makali yaliibuka kati yao na vita ikaanza.

Crime scene

Hali ya mshtuko ilitanda katika eneo la Kamakwa kaunti ya Nyeri usiku wa Jumanne baada ya jamaa mmoja kuua ndugu  yake kwa upanga kufuatia mzozo uliohusisha kiti aina ya sofa.

Elias Muriithi Kariuki, 36, anaripotiwa kukata ndugu yake mkubwa Joseph Maina  kichwani kwa kutumia upanga mkali kabla ya kujisalimisha kwa polisi.

Kulingana na DCI, Maina alikuwa ametumwa na mama yao kuenda kwa ndugu yake mdogo kuchukua sofa ambayo alikuwa amechukua  wakati malumbano makali yaliibuka kati yao na vita ikaanza.

Wakati vita kati ya wawili hao ilikuwa imenoga, Muriithi anaripotiwa kuchukua upanga mkali kutoka kwa nyumba yake na kumkata ndugu yake mkubwa kichwani mara kadhaa na kumuacha akiwa hali mahututi.

Majirani walipokuwa wanafanya juhudi kujaribu kuokoa maisha ya Maina, Muriithi alifululiza moja kwa moja hadi kituo cha polisi cha Mathari na kujisalimisha kwa kuhofia kupigwa kitutu na wakazi waliokuwa wamejawa na ghadhabu.

Polisi walipofika kwenye eneo la tukio baada ya kupokea taarifa walipata mwili wa marehemu ukiwa umelala kwenye dibwi la damu yake.

Muriithi alikamatwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni kujibu mashtaka ya mauaji yanayomkabili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved