logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa anajisi mtoto wa miaka 5 na kumpatia shilingi 15 ili anyamaze kisha kutoweka Makueni

Peter Nzinzi Musyoki 40, anaripotiwa kutekeleza kitendo hicho cha unyama mnamo Jumatatu mida ya asubuhi wakati mtoto huyo alikuwa ametumwa kuchukua maziwa ya kutengezea kiamsha kinywa kwa jirani yao.

image
na Radio Jambo

Burudani14 September 2021 - 02:17

Muhtasari


•Musyoki alivizia mtoto huyo kwa njia kisha kumpeleka katika kichaka kilicho karibu ambako alimtendea unyama huo.

•Baada ya kutekeleza hayo jamaa huyo anasemekana kupatia mtoto yule shilingi kumi na tano ili aweze kubaki kimya kuhusiana na kilichokuwa kimetendeka.

crime scene

Polisi  wanasaka jamaa mmoja anayedaiwa kutoweka baada ya kanajisi msichana wa miaka mitano katika kijiji cha Kilia, eneo la Mukaa, kaunti ya Makueni.

Peter Nzinzi Musyoki 40, anaripotiwa kutekeleza kitendo hicho cha unyama mnamo Jumatatu mida ya asubuhi wakati mtoto huyo alikuwa ametumwa kuchukua maziwa ya kutengezea kiamsha kinywa kwa jirani yao.

Kulingana na DCI, Musyoki alivizia mtoto huyo kwa njia kisha kumpeleka katika kichaka kilicho karibu ambako alimtendea unyama huo.

Baada ya kutekeleza hayo jamaa huyo anasemekana kupatia mtoto yule shilingi kumi na tano ili aweze kubaki kimya kuhusiana na kilichokuwa kimetendeka.

Hata hivyo, mama ya mhasiriwa ambaye alijawa na wasiwasi baada ya kuona bintiye alimkimbiza katika hospitali ya Kilungu Level 4 ambako alihudumiwa na ikathibitishwa kwamba alikuwa amenajisiwa.

Wapelelezi wametoa ombi kwa yeyote ambaye ana ripoti yeyote kuhusu aliko mshukiwa huku wakitia juhudi kumpata haraka iwezekanavyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved