logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nampeza! Wambui Collymore amtakia marehemu mumewe heri za siku ya kuzaliwa

Wambui amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Safaricom Michael Joseph  kwa kumtambulisha Collymore maishani mwake.

image
na Radio Jambo

Burudani13 January 2022 - 10:25

Muhtasari


•Wambui amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Safaricom Michael Joseph  kwa kumtambulisha Collymore maishani mwake.

Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Safaricom Bob Collymore na mkewe Wambui Kamiru-Collymore katika hafla ya awali.

Bi Wambui Kamiru Collymore amemtakia marehemu mume wake Bob Collymore heri za siku ya kuzaliwa.

Wambui ametumia ukurasa wake wa Twitter kumsherehekea bosi huyo wa zamani wa Safaricom takriban miaka miwili unusu tangu kuaga kwake.

"Heri za kuzaliwa Bw. Collymore @bobcollymore" Wambui ameandika na kuambatisha ujumbe wake na picha ya mume wake marehemu.

Wambui amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Safaricom Michael Joseph  kwa kumtambulisha Collymore maishani mwake. 

Joseph alikuwa ametakia marehemu Collymore heri za siku ya kuzaliwa na kusema kwamba anampeza sana.

"Capricon mwenzangu! Nampeza sana" Michael Joseph aliandika.

Wambui alikiri kwamba anampeza sana marehemu mumewe pia.

"Nimemkumbuka pia MJ. Asante kwa kumleta katika maisha yangu. Na, kwa kweli, siku ya kuzaliwa yenye furaha kwako pia! " Wambui alimjibu Michael Joseph.

Hivi leo (Januari 13) Collymore angekuwa anasherehekea kuhitimu miaka 63 iwapo bado angekuwa hai.

Collymore aliaga duniua mnamo Julai 1, 2019 akiwa nyumbani kwake Kitusuru baada ya kuugua saratani kwa kipindi kirefu.

Aliaga akiwa na umri wa miaka 61 na kuacha mjane mmoja na watoto wanne.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved