logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hamisa Mobetto azungumzia madai ya mahusiano ya kimapenzi kati yake na Rick Ross

Mpenzi huyo wa zamani wa staa wa Bongo Diamond Platnumz alisisitiza kwa sasa anaangazia kukuza nembo yake na kujipatia utajiri zaidi.

image
na Radio Jambo

Burudani18 January 2022 - 05:28

Muhtasari


•Wawili hao wamedaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi kufuatia matendo yao ya kutiliwa shaka kwenye mitandao ya kijamii.

•Mpenzi huyo wa zamani wa staa wa Bongo Diamond Platnumz alisisitiza kwamba kwa sasa anaangazia kukuza nembo yake na kujipatia utajiri zaidi.

Mwanamuziki na mwigizaji mashuhuri kutoka Tanzania Hamisa Mobetto amepuuzilia mbali uwepo wa mahusiano ya kimapenzi kati yake na rapa wa Marekani William Leonard Roberts II almaarufu kama Rick Ross.

Wawili hao wamedaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi kufuatia matendo yao ya kutiliwa shaka kwenye mitandao ya kijamii.

Alipokuwa kwenye mahojiano na NTV, mlimbwende huyo aliweka wazi kwamba Rick Ross ni rafiki wake wa karibu na mshirika wake wa kibiashara.

“Sisi ni kama familia kubwa na tumefanya vitu vingi pamoja ambavyo nitakuwa navizindua hivi karibuni’’, Mobetto alisema.

Mobetto alizungumza wakati wa ziara yake nchini Kenya ambapo anahusika na kazi za hisani katika mtaa wa Kayole,  Nairobi.

Mpenzi huyo wa zamani wa staa wa Bongo Diamond Platnumz alisisitiza kwamba kwa sasa anaangazia kukuza nembo yake na kujipatia utajiri zaidi.

Mobetto pia alifichua kwamba amefanya kolabo ya muziki na Bien wa Sauti Sol pamoja na Otile Brown ambazo zitakuwa zinaachiliwa hivi karibuni.

Takriban miezi miwili iliyopita wasanii hao walizua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kuonekana wakijiburudisha pamoja katika maeneo mbalimbali ya burudani jijini Dubai.

Matendo ya Mobetto na Rick Ross waliacha wafuasi wao na maswali chungu nzima huku wengi wakiamini kuna kitu kinachoendelea kati yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved