logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mama Diamond asifia aliyekuwa mpenzi wa mwanawe, Wema Sepetu

Ingawa kumekuwa na tetesi kwamba Diamond anatoka kimapenzi na msanii Zuchu huku uvumi huo ukiwavutia wengi na kutaka kujua kama ni ukweli wasanii hao wanachumbiana

image
na

Burudani27 January 2022 - 06:35

Muhtasari


•Ingawa kumekuwa na tetesi kwamba Diamond anatoka kimapenzi na msanii Zuchu huku uvumi huo ukiwavutia wengi na kutaka kujua kama ni kweli  wasanii hao wanachumbiana

•Mama Dangote ameonekana kuwa na mtanzamo tofauti huku siku Jumatanne alichapisha video kwenye ukurasa wake wa Instagram ambako aliionekana akiwa amevalia dera alilonunuliwa na Wema Sepetu.

mama dangote

Mamake Diamond, Sanura Kasimu almaarufu Mama Dangote amesifia aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Mwanawe, Wema Sepetu.

Ingawa kumekuwa na tetesi kwamba Diamond anatoka kimapenzi na msanii Zuchu huku uvumi huo ukiwavutia wengi na kutaka kujua kama ni kweli wasanii hao wanachumbiana. 

Mama Dangote ameonekana kuwa na mtanzamo tofauti na siku Jumanne alipakia video kwenye ukurasa wake wa Instagram ambako aliionekana akiwa amevalia dera alilonunuliwa na Wema Sepetu.

 Kulingana naye, vazi hilo alinunuliwa na Wema Sepetu siku ya kuadhimisha kuzaliwa kwake na inabaki kama kumbukizi maishani.

Mashabiki  wa wasanii hao wamebaki njia panda wakishindwa kwa nini Mama Dangote anaonekana kuwa hazungumzii mahusiano ya mwanawe na Zuchu ilhali Mama wa Zuchu alizungumza kuhusu habari za mwanawe na Diamond.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved