logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Joyce Omondi achukua nafasi ya Kambua runinga ya Citizen

Mtangazaji Joyce Omondi amekuwa wa hivi punde kuajiriwa na runinga ya Citizen ili kuziba nafasi ya mtangazaji Kambua

image
na Radio Jambo

Habari03 February 2022 - 05:39

Muhtasari


• Mtangazaji Joyce Omondi amekuwa wa hivi punde kuajiriwa na runinga ya Citizen ili kuziba nafasi ya mtangazaji Kambua

• Omondi amepata kazi katika kituo hicho baada ya kuondoka kwenye kituo cha runinga cha Switch mwishoni mwa mwaka 2020

• Atakuwa anashirikiana na mcheza santuri Gee Gee na mwanamuziki wa injili ambaye pia ni mtangazaji, Timeless Noel.

Mtangazaji Joyce Omondi amekuwa wa hivi punde kuajiriwa na runinga ya Citizen ili kuziba nafasi ya mtangazaji Kambua aliyeondoka runingani humo baada ya kuwa mtangazaji wa kipindi cha injili, Rauka kwa zaidi ya mwongo mmoja.

Omondi ambaye ni mkewe mwanahabari Wahiga Mwaura ambaye pia anafanya kazi katika runinga hiyo ya Citizen kama mhariri mkuu, amepata kazi katika kituo hicho baada ya kuondoka kwenye kituo cha runinga cha Switch mwishoni mwa mwaka 2020, Kituo ambacho kilikuja kufungwa mwaka mmoja baadaye mwishoni mwa mwaka 2021.

Omondi hatakuwa mgeni katika runinga ya Citizen kwani aliwahi fanya kazi huko na aliondoka miaka minane iliyopita kwa kile alichokitaja kuwa ni kujiendeleza kimasomo nchini Marekani.

Katika tangazo lililopeperushwa kwenye runinga ya Citizen, Omondi anatarajiwa kurejelea kuongoza kipindi cha Rauka ambacho alikuwa akiongoza kabla ya kuondoka zake kwenda Marekani.

Atakuwa anashirikiana na mcheza santuri Gee Gee na mwanamuziki wa injili ambaye pia ni mtangazaji, Timeless Noel.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved