logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kivutha Kibwana akashifu madharau ndani ya Azimio

Kivutha Kibwana amesema lazima maslahi yao yashughulikiwe ndiposa wasalie ndani ya Azimio.

image
na Radio Jambo

Burudani07 April 2022 - 08:03

Muhtasari


• Kivutha Kibwana amekashifu uongozi wa vuguvugu la Azimio la Umoja kwa kutoshughulikia maslahi yao.

• Amekanusha madai kwamba vyama vyao ni vidogo, na kwamba wana mchango mkubwa mbele ya uchaguzi mkuu mwezi Agosti.

Gavana wa kaunti ya Makueni ambaye pia ni kinara wa chama cha Muungano, Kivutha Kibwana amezungumza mazito kuhusu madharau wanayoonyeshwa ndani ya muungano wa Azimio la Umoja One Kenya Alliance.

Akizungumza na wanahabari, Kibwana alionyesha kughadhabishwa kwake kwa kile alichokitaja kuwa uongozi wa vuguvugu hilo kukosa kuona mchango wao katika mchakato wa kushinda uchaguzi wa Agosti 9.

Kibwana alisema kwamba alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuaminia katika ndoto ya Azimio hata kutupilia mbali azma yake ya urais, hivyo basi anapaswa kupewa heshima anayostahiki.

Alishikilia kwamba maslahi ya vyama vyote kwenye muungano huo lazima yashughulikiwe kwa usawa.

"...Jambo ambalo lipo wazi ni kwamba huwezi kujua chama kikubwa na kidogo kwa sasa, tusubirie baada ya uchaguzi mkuu," Kivutha Kibwana alisema.

Kulingana naye, walitaka manifesto za vyama vyote kushirikishwa kwenye ajenda za muungano huo ili kuhakikisha wahusika wote wanathaminiwa.

Kwa sasa wafuasi wake watalazimika kusubiri kuona iwapo ataendelea kusalia ndani ya Azimio la Umoja One Kenya Alliance ama ataghairi uamuzi huo.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved