logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DP Ruto aomboleza kifo cha bintiye aliyekuwa seneta wa Machakos Johnson Muthama

Alimtaja Janet kuwa ni mtu ambaye atakumbukwa kwa bidii, uaminifu na kutegemewa.

image
na Radio Jambo

Burudani26 April 2022 - 12:06

Muhtasari


  • Habari za kifo chake zilitangazwa kwa mara ya kwanza na Naibu Rais William Ruto mnamo Jumanne

Binti ya Mwenyekiti wa chama cha United Democratic Alliance Johnson Muthama Janet Nthoki amefariki.

Habari za kifo chake zilitangazwa kwa mara ya kwanza na Naibu Rais William Ruto mnamo Jumanne.

Alimtaja Janet kuwa ni mtu ambaye atakumbukwa kwa bidii, uaminifu na kutegemewa.

"Upendo na maombi yetu kwa Mwenyekiti wa UDA Johnson Muthama kwa kumpoteza bintiye mpendwa Janet Nthoki Nduya. Alikuwa mwanamke mwenye bidii, anayewajibika na mwaminifu ambaye atakumbukwa kwa fadhili na kutegemewa kwake."

Mkuu wa pili amewapa rambirambi familia ya aliyekuwa seneta wa Machakos.

"Familia, ndugu, jamaa na marafiki wapate nguvu ya kupita katika maumivu haya. Pumzika kwa Amani Janet."

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved