logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilimpeleka kidosho wa mume wangu, kumtambulisha kwao-Mwanadada asimulia

Lakini nataka turudiane kwani washaachana na mwanamke huyo baada yake kumtesa

image
na Radio Jambo

Burudani05 May 2022 - 05:39

Muhtasari


  • Katika kitengo cha patanisho Bi Lucy alituma ujumbe apatanishwe na mumewe Ng'ang'a wa miaka miwili, ambaye walitengana  baada ya mumewe kuoa mke wa pili
Gidi na Ghost asubuhi

Katika kitengo cha patanisho Bi Lucy alituma ujumbe apatanishwe na mumewe Ng'ang'a wa miaka miwili, ambaye walitengana  baada ya mumewe kuoa mke wa pili.

Kulingana na Lucy, alimpigia mumewe simu na ikapokelewa na mwanamke huyo,kisha akampeleka kwa mumewe.

"Naomba nipatanishwe na mume wangu ambaye tulitengana mwaka jana Agosti, baada yake kuoa mwanamke mwingine

Nilijua kwamba ana mwanamke mwingine baada ya kumpigia simu na mwanamke huyo kupokea simu yake,alikuwa ananitesa baada ya kuniacha mashambani, nilimpigia mwanamke huyo na kumleta nyumbani kwa mume wangu

Lakini nataka turudiane kwani washaachana na mwanamke huyo baada yake kumtesa kama alivyokuwa ananitesa."

Baada ya kufanya juhudi za kumfikia mumewe ili waweze kupatana na Lucy,mumewe alikata simu na wala hakuzungumza lolote.

Kwa mengi zaidi tembelea Radiojambo Youtube.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved