logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wawili wafariki katika ajali ya barabara iliyohusisha gari la kampeni la gavana Kinyajui

Mhudumu wa bodaboda na abiria wake mmoja ndio waliopoteza maisha.

image
na Radio Jambo

Burudani24 May 2022 - 04:22

Muhtasari


•Mhudumu wa bodaboda na abiria wake mmoja nwalipoteza maisha yao baada ya gari hilo  kupoteza mwelekeo na kugonga pikipiki yao.

•Gavana Kinyajui alisema watu wengine wawili walionusurika kwenye ajali hiyo wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja ya Nakuru.

Gari la kampeni la gavana Kinyajui lililohusika kwenye ajali

Watu wawili walifariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha gari la kampeni la gavana wa Nakuru Lee Kinyajui na bodaboda.

Mhudumu wa bodaboda na abiria wake mmoja ndio waliopoteza maisha baada ya gari hilo lililokuwa likiendeshwa na dereva wa kike kupoteza mwelekeo na kugonga pikipiki yao katika eneo la Free Area kwenye barabara Nairobi-Nakuru.

Gavana Kinyajui kupitia taarifa alisema ajali hiyo ilitokea Jumatatu mwendo wa saa tano asubuhi huku akifariji familia za waliopoteza maisha yao. Alisema watu wengine wawili walionusurika kwenye ajali hiyo wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja ya Nakuru.

"Tunasikitika kutangaza kuwa watu wawili walipoteza maisha huku wawili walionusurika wakiendelea kupokea matibabu. Rambirambi zetu za dhati kwa familia za marehemu. Wakati huo huo, tunahakikisha kwamba waathirika wote wanapewa huduma ya matibabu inayostahili," Kinyajui alisema  kupitia Facebook.

Gavana huyo wa muhula wa kwanza pia alitumia fursa hiyo kuhamasisha watu kuhusu usalama wa barabarani na kuwaagiza madereva kumakinika zaidi.

Kinyajui ambaye alichaguliwa kama gavana wa Nakuru katika chaguzi za 2017 anatetea wadhifa wake kwa tikiti ya Jubilee.

Ni mmoja wa wanasiasa kumi na wawili ambao walihojiwa na jopo la kuteua mgombea mwenza wa muungano wa Azimio mapema mwezi huu.

Kinyajui ni miongoni mwa wandani wa rais Kenyatta ambao wameendelea kuwa waaminifu kwa serikali yake katika muhula huu wake wa mwisho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved