logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matiang'i: Hatutazima mitandao wakati wa uchaguzi

“…lakini hii haitatushawishi kuchukua hatua za kurudi nyuma kama kuzima mtandao

image
na Radio Jambo

Burudani09 June 2022 - 08:54

Muhtasari


  • “…lakini hii haitatushawishi kuchukua hatua za kurudi nyuma kama kuzima mtandao wakati wa uchaguzi

Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i amesema serikali haitazima mtandao wakati wa uchaguzi.

Katika wiki zilizopita, kampeni za Kenya zimekuwa motomoto huku wanasiasa wakidai kuna jaribio la kuingilia uchaguzi kupitia wizara ya ICT. Matiang'i alidai kuwa wameshutumiwa kwa kila aina ya mambo.

“…lakini hii haitatushawishi kuchukua hatua za kurudi nyuma kama kuzima mtandao wakati wa uchaguzi kwani tunaheshimu haki za wote,” alisema Jumatano jioni.

"Tunakaribia uchaguzi na mjadala mkubwa zaidi ni kuhusu jinsi tutakavyoishi sisi kwa sisi katika enzi ya habari za uwongo na matumizi mabaya yasiyo na kifani ya mitandao ya kijamii." Alisema serikali haitachukua hatua vinginevyo akiongeza kuwa serikali inaheshimu uhuru wa Wakenya.

"Hakuna kiasi cha matusi au ukosoaji kitakachojaribu serikali kiasi cha kufikia vitendo vya kuingilia uhuru wa Wakenya."

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved