logo

NOW ON AIR

Listen in Live

CJ Koome aeleza kwa nini CDF si halali

"Hivi majuzi katika Kesi ya CDF (2022), Mahakama ya Juu ilisema kuwa ni kinyume cha sheria

image
na Radio Jambo

Burudani21 September 2022 - 18:13

Muhtasari


  • Jaji Mkuu wakati huo huo alitaja ugatuzi kuwa mradi wa kikatiba ambao lazima ulindwe kwa gharama yoyote

Jaji Mkuu Martha Koome amefichua sababu zilizofanya Mahakama ya Juu kuharamisha Hazina ya Maendeleo ya Eneo bunge (CDF) kuwa haramu.

Koome, akihutubia Maseneta siku ya Alhamisi mjini Naivasha, alisema kwamba hazina hiyo kitita hicho kinakiuka mgawanyiko wa majukumu kati ya serikali za kitaifa na kaunti.

CJ Koome, ambaye alikuwa mmoja wa wazungumzaji katika kikao hicho Jumatano, alitoa wito kwa maseneta kuchukua jukumu kulinda mamlaka yao ya katiba ya kusimamia vitengo vilivyogatuliwa.

Koome alitumia fursa hiyo kufichua kwamba ni kwa sababu hiyo hiyo ambapo Mahakama ya Juu ilitangaza CDF kuwa si halali.

"Hivi majuzi katika Kesi ya CDF (2022), Mahakama ya Juu ilisema kuwa ni kinyume cha sheria kugawia CDF fedha kabla ya mgawanyo wa mapato kati ya serikali ya kitaifa na ya kaunti," alisema Koome.

"Isitoshe, ilikuwa ni msimamo wa Mahakama kwamba inakiuka mgawanyiko wa majukumu kati ya serikali za kitaifa na kaunti kuruhusu CDF, chombo muhimu cha serikali ya kitaifa, kutekeleza majukumu yaliyogawiwa kwa kaunti."

Pamoja na kwamba CDF ni batili, wabunge hao sasa wanatumia Mfuko wa Taifa wa Maendeleo ya Jimbo la Serikali (NGCDF), ambao kwa mujibu wa Mtendaji Mkuu wa mfuko huo, Yussuf Mbuno sasa watatumia fomula mpya itakayonufaisha majimbo yenye wakazi wengi na maeneo ambayo yana watu wachache.

Jaji Mkuu wakati huo huo alitaja ugatuzi kuwa mradi wa kikatiba ambao lazima ulindwe kwa gharama yoyote.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved