logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hongera! Amos Kipruto anyakua dhahabu katika London Marathon

Kipruto alikimbia kwa dhamira kubwa na kuvunja kanda kumaliza kwa masaa 2:04:39.

image
na Radio Jambo

Burudani02 October 2022 - 12:15

Muhtasari


• Leul Gebresilase wa Ethiopia aliibuka wa pili kwa saa 2:05.12 huku mshindi wa medali ya shaba ya Olimpiki, Bashir Abdi kutoka Ubelgiji akifunga orodha ya tatu bora.

Amos Kipruto asherehekea na bendera ya taifa baada ya kushinda shaba wakati wa mbio za marathon za wanaume

Amos Kipruto aliibuka mshindi katika mbio za wanaume za London Marathon 2022 Jumapili, wiki moja baada ya Eliud Kipchoge kuiba vichwa vya habari mjini Berlin.

Mwanariadha huyo kutoka Kenya alikimbia kwa dhamira kubwa na kuvunja kanda kumaliza kwa masaa 2:04:39.

 Leul Gebresilase wa Ethiopia aliibuka wa pili kwa saa 2:05.12 huku mshindi wa medali ya shaba ya Olimpiki, Bashir Abdi kutoka Ubelgiji akifunga orodha ya tatu bora.

Akizunguka msururu wa mwisho kupita Kasri la Buckingham, Kipruto alichagua raundi ya mbali, lakini alikuwa tayari amepata ushindi.

Akifikia alama ya 40km, Kipruto alitumia 1:58:27 na wakati huo ilionekana kufikia muda wake bora, pamoja na rekodi ya mashindano hayo.

Hata hivyo, alikimbia kwa urahisi na uwezo bidii kubwa isiyoweza kupingwa, akiwaacha Gebresilase, Abdi na Kinde wakigombania pumzi nyuma yake.

Ni Gebresilase na Abdi pekee aliweza kushikamana na Mkenya huyo katika mwendo wake wa kasi huku kundi lililobaki likisahaulika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved