logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jimal amjibu mtu aliyesema anajipendekeza kwa wanasiasa,"wewe kwa landlord!"

“Unapenda kujipendekeza kwa wanasiasa,” mtumizi wa Instagram kwa jina Bentah Johns alimwambia bila woga.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 October 2022 - 12:12

Muhtasari


• “Wewe unapenda kujipendekeza kwa mwenye nyumba,” Jimal alijibu

Jimal Rohosafi akiwa na spika wa bunge la kitaifa

Mfanyibiashara maarufu katika sekta ya matatu Jimal Rohosafi kwa mara nyingine amejipata katika mzozo mkali na watumizi wa mtandao wa Instagram.

Jimal alipakia picha wakiwa na spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula na kusema kwamba ilikuwa ni Jumapili laini yenye utulivu ambapo alikuwa anapunga upepo na kiongozi huyo wa bunge.

Mashabiki na watumizi mbali mbali walimjia juu huku wengine wakimsuta kwamba wanamwelewa kupunga upepo na kila mtu kwa sababu ni mpweke, haswa kufuatia kusambaratika kwa mahusiano yake na aliyekuwa mkewe, Amira.

Mwingine pia alimkandia kavu kwa kumwambia kwamba ana mazoea ya kujipendekeza kwa kila mtu ili kupata tu kuzungumziwa kwenye mitandao ya kijamii.

“Unapenda kujipendekeza kwa wanasiasa,” mtumizi wa Instagram kwa jina Bentah Johns alimwambia bila woga.

Kati ya maombi mbali mbali yenye masimango makali, hili lilionekana kuwa kisu kikali kilichogusa mfupa wa muundi wa guu la Jimal ambaye alishindwa kujizuia na kujibu mipigo. Alimwambia mwanadada huyo kwamba ni heri yeye anapenda kujipendekeza kwa wanasiasa ila huyo yeye anajipendekeza kwa mwenye nyumba ya kupanga.

“Wewe unapenda kujipendekeza kwa mwenye nyumba,” Jimal alijibu huku watu wakicheka kwa jibu hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved