logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Daddy Owen hatimaye afunguka kwa nini alimkataa Pritty Vishy

"Sifa zingine ako sawa. Kama hajalelewa ushago hapana," alisema.

image
na Radio Jambo

Burudani09 November 2022 - 03:56

Muhtasari


•Owen alisema kuzaliwa na kulelewa mjini kwa kipusa huyo ambaye hujitambulisha kama 'Kienyeji Pro Max' kulimuondoa kwenye orodha ya wanawake waliohitimu kuwa mkewe.

•Mwanamuziki huyo mkongwe alisisitiza kuwa mwanadada atakayekuwa mke wake ni sharti awe amelelewa kijijini.

Mwimbaji wa nyimbo za injili Owen Mwatia almaarufu Daddy Owen ameweka wazi kwamba aliyekuwa mpenzi wa mwanamuziki Stivo Simple Boy, Purity Vishenwa almaarufu Pritty Vishy hakufikia sifa za kuwa mke wake.

Katika mahojiano na Plug TV, Owen alisema kuzaliwa na kulelewa mjini kwa kipusa huyo ambaye hujitambulisha kama 'Kienyeji Pro Max' kulimuondoa kwenye orodha ya wanawake waliohitimu kuwa mkewe.

"Pritty Vishy hajalelewa ushago (kijijini). Hiyo ndio inamuondoa. Sifa zingine ako sawa. Kama hajalelewa ushago hapana," alisema.

Mwanamuziki huyo mkongwe alisisitiza kuwa mwanadada atakayekuwa mke wake ni sharti awe amelelewa kijijini.

Siku chache zilizopita Pritty Vishy alijitolea kuwa mke wa  Daddy Owen baada ya mwimbaji huyo kudaiwa anatafuta mwanamke 'kienyeji'.

Kipusa huyo mwenye umri wa miaka 21 alitoa ombi kwa watu wanaoweza kumfikia msanii huyo kumwambia kwamba yupo radhi kuwa mke wake kwani tayari kigezo cha kuwa kienyeji tayari anacho.

"Si mtu amwambie Daddy Owen kwa niaba yangu kuwa nipo singo na bila vipodozi mimi ni mweusi wa asili. Mimi si rangi ya mkorogo kwa sababu sijui mtu anakuwa mkorogo aje. Pia napenda maombi sana, ifikie Daddy Owen," alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Katika jibu lake, Owen alimwambia Vishy kuwa anapaswa kusubiri kwa kuwa foleni ni ndefu sana na bado hajafikiwa.

"Huyu mwambieni line ni ndeefu,hajafikiwa bado..lakini kama marathon tutazawadi kila mmoja atakaye vuka laini," Alisema.

Vishy alionekana kughadhabishwa na jibu la mwanamuziki huyo na kukinzana na kauli yake ya awali kuwa alitaka kuwa mke wake.

“Nilikuwa namtaka lakini sasa ni kama atavuka upande wa Uganda, ni mwanaume yupi ambaye anataka kuwa na ufisadi? Nasikia hataki mwanamke ambaye yuko kwenye mtandao wa TikTok na anayeongea Kizungu kingi,” Vishy alisema.

Daddy Owen hata hivyo sasa ameweka wazi kuwa bado hajajitosa kwenye pilka pilka za kutafuta mwanamke wa kuchumbia na kuoa.

"Mimi ni mwanaume, siwezi kutangaza kuwa natafuta mwanamke. Mimi ni simba, nikitaka mwanamke nitaenda huko nje na niwinde," alisema.

Awali alikuwa amesema kwamba mama yake amekuwa akimpa shinikizo la kutafuta mwanamke wa kuwa akitembea naye nyumbani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved