logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanaume asimulia kubakwa na 'maid' akiwa na miaka 20, "aliniweka juu ya meza!"

Kutokana na kitendo cha kulazimishwa kufanya mapenzi na msichana wa kazi za ndani, msichana yule alipata mimba

image
na Radio Jambo

Burudani19 November 2022 - 07:06

Muhtasari


• Alisema kwamba siku moja akirejea nyumbani alimpata mjakazi huyo ambaye hawakuwa na mazoea ya kuzungumza naye sana ameandaa chai ya jioni na vitafunio.

• Mjakazi yule kwa weledi mkubwa alimsogelea karibu na kuanza kumlisha kabla ya kumuinua na kumketisha mezani.

Mwathirika wa ubakaji, Otieno Onyango

Mwanaume mmoja kwa jina Onyango Otieno amezua gumzo kweney mitandao ya kijamii baada ya kuonekana kwenye Makala ya kipekee runingani NTV usiku wa Ijumaa akisimulia jinsi mjakazi wa nyumbani alimbaka akiwa na miaka 20.

Kulingana na Otieno, mwaka 2008 akiwa na miaka 20 mfanyikazi wa ndani nyumbani kwao alimlazimisha kushiriki tendo la ndoa naye katika kile ambacho alikieleza kuwa ulikuwa ni ubakaji.

“Mwaka 2008 nilikuwa na miaka 20, nilikuwa mwanafunzi wa kidato cha 5 katika shule moja nchini Uganda. Ilikuwa Desemba wakati wazazi wangu walimwajiri mjakazi mpya na Januari wakati kila mtu alienda shuleni na kazini, tulibaki mimi na mjakazi pekee nyumbani,” Otieno alieleza.

Alisema kwamba siku moja akirejea nyumbani alimpata mjakazi huyo ambaye hawakuwa na mazoea ya kuzungumza naye sana ameandaa chai ya jioni na vitafunio ambavyo alimpakulia ili kula.

Kilichomshangaza ni kwamba binti yule kijakazi alitaka kuketi karibu naye ii wanywe chai kwa pamoja.

“Alitaka kunisogezea kwa ukaribu kabisa mpaka kufikia kiwango cha kutaka kunilisha mandaazi. Nakumbuka akinibeba na kuniweka juu ya meza na hili sikuwahi kulisimulia kwa mtu yeyote,” Otieno alisimulia.

Baadae yule mwanadada alipata ujauzito kutokana na kitendo kile cha kulazimisha mapenzi na kijana wa watu na mamake ndiye alikuja kumpigia simu baadae akimuuliza iwapo mjakazi alimwambia ni mjamizito.

Kando na hapo, pia mamake alimwambia kwamba mjakazi yule alimwambia alikuwa na uonjwa wa zinaa. Kulingana na Otieno, hakuweza kuripoti kitendo hicho kwa mtu yeyote kwa sababu kipindi hicho hakuwa anafahamu kwamba ulikuwa ni unyanyasaji wa kingono na miaka 10 baadae aliamua kutafuta huduma za ushauri nasaha kaam njia moja ya kumponya kutokana na kitendo hicho kilichomtokea akiwa na miaka 20.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved