logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aingia kwenye klabu ya jinsia moja na bunduki, aua 5 na kujeruhi 18 Colorado Marekani

Mtu mmoja aliyekuwa na risasi alishambulia klabu hiyo

image
na Radio Jambo

Burudani21 November 2022 - 04:21

Muhtasari


• Hii ni baada ya mtu aliyekuwa na silaha kushambulia kwa risasi klabu ya wapenzi wa jinsia moja.

Takriban watu watano wameuawa na wengine 18 kujeruhiwa katika jimbo la Colorado nchini Marekani Jumamosi usiku. 

Hii ni baada ya mtu aliyekuwa na silaha kushambulia kwa risasi klabu ya wapenzi wa jinsia moja.

Polisi walisema mshukiwa, kwa jina Anderson Lee Aldrich, 22, amekamatwa na anatibiwa majeraha.

Watu wawili "mashujaa" kwenye kilabu walifanikiwa kumdhibiti mshambuliaji, polisi walisema.

Club Q, huko Colorado Springs, ilitoa taarifa kwenye Facebook ikisema "imehudhunishwa na shambulio lisilo na maana kwa jamii yetu".

Polisi wa Colorado Springs waliwataka watu kuwa na subira wakati wanafanya kazi ya kutambua waathiriwa na kukamilisha idadi ya majeruhi. Mshukiwa huyo alipatikana ndani ya klabu hiyo wakati polisi walipoingia.

Mwaka wa 2016, watu 49 waliuawa na zaidi ya 50 kujeruhiwa kwa risasi kwenye klabu ya usiku ya wapenzi wa jinsia moja huko Orlando, Florida. Kwa wakati huo hayo yalikuwa mauaji mabaya zaidi ya watu wengi kwa wakati mmoja katika historia ya Marekani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved