logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneti yapendekeza kamati ya watu 11 kumchunguza gavana Kawira

Kamati ya Seneti ya Biashara iliomba Bunge kuidhinisha majina 11 ambayo imependekeza kuketi kwenye jopo.

image
na

Burudani20 December 2022 - 12:29

Muhtasari


•Kamati ya Biashara ya Seneti iliomba Bunge kuidhinisha majina 11 ambayo imependekeza kuketi kwenye jopo hilo.

•Miongoni mwa maseneta ambao majina yao yametajwa kuketi katika jopo hilo ni kinara wa wengi Boni Khalwale , Jackson Mandago , Karungo Thangwa, na Ali Roba.

Uongozi wa Seneti umependekeza kuundwa kwa kamati maalum ya kuchunguza mashtaka dhidi ya gavana wa Meru aliyezingirwa Kawira Mwangaza.

Katika kikao kilichofanyika Jumanne asubuhi, Kamati ya Biashara ya Seneti iliomba Bunge kuidhinisha majina 11 ambayo imependekeza kuketi kwenye jopo hilo.

Kiongozi wa Wengi katika Seneti Aaron Cheruiyot ameratibiwa kutoa hoja wakati wa kikao maalum ya kuundwa kwa kamati hiyo Jumanne alasiri.

“Seneti inaazimia kuunda kamati maalum kuchunguza mapendekezo ya kuondolewa afisini kwa Gavana wa Kaunti ya Meru,” hoja hiyo inasomeka kwa sehemu.

Miongoni mwa maseneta ambao majina yao yametajwa kuketi katika jopo hilo ni kinara wa wengi Boni Khalwale (Kakamega), Jackson Mandago (Uasin Gishu), Karungo Thangwa (Kiambu) na Ali Roba (Mandera).

Maseneta wengine ni Esther Okenyuri (wa kuteuliwa), Peris Tobiko (wa kuteuliwa), Eddy Oketch (Migori), Joseph Kamau (Lamu), Edwin Sifuna (Nairobi), Agnes Kavindu (Machakos) na Johnes Mwaruma (Taita Taveta).

Kifungu cha 33 cha Sheria ya Serikali za Kaunti kinasema kwamba Seneti inaweza kutekeleza kubanduliwa kwa gavana kupitia kamati maalum au kikao.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved