logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ Evolve kuzindua hazina ya kuwasaidia walemavu

Tamasha la kwanza linatarajiwa kufanyika Februari 12, 2023,

image
na Radio Jambo

Burudani27 January 2023 - 14:29

Muhtasari


  • Tamasha hizo zimepangwa kufanyika kila mwezi jijini Nairobi na kote nchini, na mapato kutoka kwa tukio litaelekezwa katika The Evolve Fund
DJ Evolve na Juliani

Mcheza santuri Felix Orinda anayejulikana pia kama DJ Evolve ametangaza mpango wake wa kuanzisha hazina ya  kusaidia watu wanaoishi na ulemavu.

Katika taarifa amesema hazina hiyo itawahusisha watu wanaoishi mashinani na kimataifa.

Katika taarifa yake, DJ Evolve alisema kupata nafasi ya pili, nafasi ya maisha kufuatia mkasa uliomsababishia ulemavu ilimtia moyo kuanzisha hazina ya The Evolve kusaidia watu wenye ulemavu nchini Kenya na kimataifa.

Tamasha hizo zimepangwa kufanyika kila mwezi jijini Nairobi na kote nchini, na mapato kutoka kwa tukio litaelekezwa katika The Evolve Fund

Tamasha la kwanza linatarajiwa kufanyika Februari 12, 2023, na miongoni mwa wacheza santuri ambao tayari wamethibitishwa kuhudhuria tukio hilo ni pamoja na DJ Purpl,DJ Saint Kevinsky,DJ Mjay Kenya,DJ Namosky,DJ Twinn 48 miongoni mwa wacheza santuri wengine.

Ili kuchangisha fedha, DJ Evolve alishirikiana na Tufund, jukwaa la ufadhili wa watu wengi ambalo hutafuta kuwezesha watu kupata ufadhili kwa sababu tofauti, na Matukio ya Mtickets kuandaa matukio ya matamasha yaliyopewa jina la Evolution.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved