logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ombi la kutaka Koome kung’atuliwa lawasilishwa kwa JSC

Jaji mkuu hafai kushikilia wadhifa huo na anapaswa kuondolewa madarakani.

image
na Radio Jambo

Burudani01 February 2024 - 08:56

Muhtasari


• Mlalamishi, Michael Kojo Otieno, anadai kuwa Jaji Mkuu alikosa kufuata sheria katika kuwateua wanachama wa mahakama ya rufaa ya ushuru. 

Ombi limewasilishwa mbele ya Tume ya Huduma za Mahakama (JSC) kutaka Jaji Mkuu Martha Koome aondolewe afisini. 

Mlalamishi, Michael Kojo Otieno, anadai kuwa Jaji Mkuu alikosa kufuata sheria katika kuwateua wanachama wa mahakama ya rufaa ya ushuru. 

Kojo anahoji kuwa Koome hakuwa muwazi na kuwa aliwabagua watu ambao walikuwa wametuma maombi ya kuwa wanachama wa bodi. 

"Hatua za jaji mkuu katika kuteua wanachama zaidi ya mahitaji yaliyowekwa zilikiuka kifungu cha 4b cha Sheria ya Mahakama ya Rufaa ya Ushuru," Kojo anasema. 

Anasema kuwa kwa sababu za kukiuka sheria, jaji mkuu hafai kushikilia wadhifa huo na anapaswa kuondolewa madarakani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved