logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Stephen Letoo aeleza kwa nini yeye na mkewe wataenda sehemu tofauti kwa honeymoon

Letoo alieleza kuwa sio kawaida yao kufuata njia ya kawaida ya kwenda mahali sawa na mke wake.

image
na Radio Jambo

Burudani09 April 2024 - 07:51

Muhtasari


  • Letoo alionyesha nia yake ya kumwacha bibi harusi wake aamue anakotaka kwenda, huku yeye pia akichagua anakoenda.
STEPHEN LETOO

Mwanahabari wa runinga ya Citizen Stephen Letoo amewaacha mashabiki wakishangazwa na mbinu yake isiyo ya kawaida ya mipango ya honeymoon, akitangaza kuwa yeye na mchumba wake hawatakuwa na honeymoon ya kawaida baada ya harusi pamoja.

Katika mahojiano na Oga Obinna, alielezea mtazamo wake kuhusu mipango ya honeymoon, akisema kuwa sio kawaida yao kufuata njia ya kawaida ya kwenda mahali sawa na mke wake.

Badala yake, Letoo alipendekeza wazo jipya;  kila mmmoja wao angechagua eneo tofauti la kwenda honeymoon pekee yao.

Letoo alionyesha nia yake ya kumwacha bibi harusi wake aamue anakotaka kwenda, huku yeye pia akichagua anakoenda.

Alisisitiza kuwa sababu ya honeymoon ni kustarehe  baada ya uchovu wa kupanga harusi, badala ya kuhisi shinikizo la kupata mtoto nje ya nchi.

"Nilimwambia mgeni mkuu wa hiyo siku achague ni wapi anataka kwenda. Mimi Nitaenda honeymoon yangu mwenyewe na yeye ataenda yake. Honeymoon inapaswa kuwa ya kufuta jasho ambalo umepata kupitia mipango madhubuti sana.Siyo kwenda kusumbuana kutafuta mtoto ughaibuni," Letoo alieleza.

Aliangazia nia yake ya kuchagua anakoenda kulingana na matakwa ya kibinafsi, iwe ni makazi tulivu ya Maasai Mara au burudani huko Dubai.

Vivyo hivyo, alionyesha kuunga mkono uamuzi wa mke wake, hata ikiwa ataamua kusafiri na marafiki kwenda mahali tofauti

"Mimi ntachagua yangu kama ntaenda Masaai Mara ntaenda na yeye atachagua hata kama ni dubai ataenda na marafiki zake," Letoo alisema


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved