logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nigeria yabadilisha wimbo wa taifa na kurudisha wimbo uliotumika mara ya mwisho 1978

Rais Bola Tinubu ametia saini kuwa sheria Mswada wa Wimbo wa Kitaifa uliopitishwa na Bunge la Kitaifa.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2024 - 13:04

Nigeria imerejea kwa wimbo wa taifa uliotumika kabla ya 1978 baada ya Rais Tinubu kutia saini kuwa sheria.

Rais Bola Tinubu ametia saini kuwa sheria Mswada wa Wimbo wa Kitaifa uliopitishwa na Bunge la Kitaifa siku ya Jumanne.

Mswada huo unarejelea wimbo wa zamani wa taifa wa Nigeria wakati wa uhuru mnamo 1960 "Nigeria tunakupongeza."

Wimbo wa zamani wa taifa ulifutwa na jeshi mnamo 1978 na miaka 46 baada ya Rais Bola Tinubu kutia saini mswada wa kurejesha wimbo huo badala ya mpya zaidi "Arise oh compatriots."

 Rais wa Seneti, Godswill Akpabio alifichua idhini hiyo ya Rais muda mfupi uliopita katika kikao cha pamoja cha mabunge yote mawili ya Bunge la Kitaifa kuadhimisha miaka 25 ya demokrasia isiyovunjika nchini.

Awali, Naibu Spika, Baraza la Wawakilishi Benjamin Kalu aliwaagiza wabunge na wageni wanaosubiri kuwasili kwa Rais Bola Tinubu ili kupakua wimbo wa Taifa wa zamani ambao sasa ungekuwa wimbo wa taifa wa Nigeria.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved