logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matokeo rasmi ya uchaguzi Afrika kusini kutangazwa leo

ANC imekuwa na wengi katika jimbo hilo tangu mwisho wa ubaguzi wa rangi mwaka 1994.

image
na Radio Jambo

Burudani01 June 2024 - 19:23

Muhtasari


  • Chama tawala ANC kinatarajiwa kupoteza nguvu kilichoshikilia katika miongo mitatu ya siasa baada ya kupungua kwa wafuasi wake kwa kiwango kikubwa.

Matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu Afrika kusini yanatarajiwa kutangazwa Jumapili jioni, afisa mmoja wa tume anasema.

Zoezi la kuhesabu kura linaingia katika hatua ya mwisho huku 98% ya matokeo yakiwa yamepokewa tayari.

Naibu mkurugenzi mtendaji wa tume ya uchaguzi nchini Mawethu Mosery, ameiambia televisheni ya eNCA kwamba tume itakesha usiku kucha Jumamosi kukabiliana na pingamizi na maombi.

Chama tawala ANC kinatarajiwa kupoteza nguvu kilichoshikilia katika miongo mitatu ya siasa baada ya kupungua kwa wafuasi wake kwa kiwango kikubwa.

Viongozi wa ANC wajadili njia ya kusonga mbele

Chanzo cha ANC chasema kuwa maafisa saba wakuu wa ANC, akiwemo Rais Cyril Ramaphosa wanakutana kujadili njia ya kusonga mbele baada ya matokeo ya uchaguzi.

Kama ilivyo kwa nchi nzima, jimbo tajiri zaidi la Afrika Kusini la Gauteng linatazamiwa kuwa na serikali ya mseto baada ya chama cha African National Congress (ANC) kupoteza wingi wake.

Kwa 97% ya kura kukamilika kuhesabiwa, ANC imepata 35% tu ya kura – kupoteza kwa kiasi kikubwa tangu uchaguzi wa 2019 ilipopata 50%.

Bado ni chama kikubwa zaidi katika jimbo hilo, ambacho kinajumuisha jiji kubwa zaidi la Johannesburg na mji mkuu, Pretoria, lakini kitahitaji kuunda muungano.

Chama cha Democratic Alliance (DA) kiko katika nafasi ya pili, kwa asilimia 28 ya kura, kikifuatiwa na Economic Freedom Fighters (EFF) kwa asilimia 13%.

ANC imekuwa na wengi katika jimbo hilo tangu mwisho wa ubaguzi wa rangi mwaka 1994.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved