logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Mimi ni mdogo sana kupitia hili" - Mrembo GenZ alia juu ya changamoto kulea mapacha

“Mama yangu amesafiri kurudi kwake, na mume wangu hayupo nyumbani, niko peke yangu na mapacha hawa. Watoto wanalia bila kukoma, ni hali ya kutamausha sana,’ aliongeza huku akilia .

image
na MOSES SAGWE

Burudani03 November 2024 - 10:45

Muhtasari


  • Klipu hiyo iliyotumwa na mtumiaji wa TikTok @destinybellaluv, inanasa mama huyo mdogo akionekana kuzidiwa, huku mapacha wake wakilia bila kujizuia.



Mrembo wa kizazi cha Gen Z ambaye siku za hivi majuzi alikuwa mama, shukrani kwa ujio wa mapacha amechukua kwenye mitandao ya kijamii akilia kuhusu changamoto za kulea wanawe.

Katika video hiyo ambayo imevutia hisia mseto, mrembo huyo alikuwa Analia akisema kwamba yeye bado ni mchanga sana kupitia changamoto kama hiyo kwani shughuli ya kulea mapacha imekuwa mchongoja na kuupanda ndio ngoma sasa.

Alifichua kwamba alikuwa anafurahia safari yote ya ujauzito wake na hata fikira ya kuitwa mama lakini hakuwahi jua kwamba kulea mapacha ni kibarua ambacho sasa kinaelekea kumletea madhara ya afya ya kiakili.

Alisema kwamba siku za mwanzoni, mama yake ndiye alikuwa anamsaidia lakini baada ya kurudi nyumbani, amesali peke yake na wanawe mapacha, na imekuwa changamoto isiyoweza kuvumilika kwake.

Klipu hiyo iliyotumwa na mtumiaji wa TikTok @destinybellaluv, inanasa mama huyo mdogo akionekana kuzidiwa, huku mapacha wake wakilia bila kujizuia.

Katika video hiyo, anaeleza kwamba Mpenzi wake pia alikuwa hayupo, na kumwacha bila msaada wakati akijaribu kusimamia mahitaji ya kuwatunza watoto wake wachanga.

Kuchanganyikiwa na hali ya kutojiweza ya mwanamke huyo ilivutia watazamaji wengi, huku watumiaji wengi katika sehemu ya maoni wakitoa maneno yake ya kutia moyo na vidokezo kuhusu kudhibiti watoto.

“Hamjambo wapendwa, habari za asubuhi, kusema ukweli tangia saa saba usiku wa kuamkia leo, wanangu wamekuwa wakilia. Na mimi ninalia kwa sababu niko peke yangu katika nyumba hii. Na kusema kweli nimechoka,” alisema.

“Mama yangu amesafiri kurudi kwake, na mume wangu hayupo nyumbani, niko peke yangu na mapacha hawa. Watoto wanalia bila kukoma, ni hali ya kutamausha sana,’ aliongeza huku akilia pia.

Wengi walimhakikishia kwamba ni kawaida kuhisi kulemewa na kumtia moyo kuendelea licha ya changamoto.

Mtumiaji wa mtandao wa kijamii, @Aboobae♥️👑✨ aliandika, "Nakumbuka wakati najifungua, 1am mtoto wangu alikuwa akilia na nilikuwa peke yangu dhaifu sana na uchovu nilichokuwa nikisikia ni kumtupa ili upumzike vizuri."

Mtumiaji mwingine, @Mimi4luve alijibu, "Naapa si rahisi bado nipo nyumbani kwa mama yangu tuna karibu miezi 4 sio rahisi (mapacha wa kike) hata baba yangu hubeba wakati analia mpenzi wangu nahisi upo."

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved