logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gavana Sakaja aahidi barabara moja jijini Nairobi kuitwa jina la msanii E-Sir kama ukumbusho wake

Baadhi za barabara jijini Nairobi kupewa jina za wasanii washuhuri kama njia ya kuwapa heshima na kuwakumbuka.

image
na OTIENO TONNY

Burudani13 December 2024 - 15:05

Muhtasari


  • E-Sir aliyejulikana kwa jina lake halisi kama Issah Mmari alifariki tarehe 16 Machi 2003.
  • Baadhi ya ngoma zake zilizotamba ni pamoja na ‘Leo ni Leo’ na ‘Moss Moss’ ambazo bado zinazidi kutamba miaka kadhaa baada ya kifo chake.


Gavana wa kaunti ya Nairobi Johnson Sakaja ameahidi kutaja baadhi ya barabara katika kaunti anayoongoza majina ya wasanii tajika waliovuma kama njia moja ya kuwakumbuka kwajuhudi zao za kuweka msingi bora katika sekta ya usanii nchini.

Gavana huyo alisema hayo katika maadhimisho ya miaka 61 ya Jamhuri iliyoandaliwa ugani Uhuru Gardens jijini Nairobi mnamo Alhamisi gavana Sakaja akiahidi kuipa barabara moja katika mtaa wa South C jina E-Sir ambaye alikuwa msaani tajika wa rap nchini.

‘’Nimeongea na mwenzangu mheshimiwa  Jalas na tutabadilisha majina ya baadhi ya barabara jijini na kuzipatia majina ya wasanii wetu mashuhuru. Barabara iliyo katika eneo la South C itapewa jina la  E-Sir na hata ndugu yake ametutumbuiza hapa  kama njia ya kuwakumbuka na kuwapa heshima wasanii wetu mashuhuri,’’ Alisema Sakaja.

Msanii tajika nchini David Mathenge maarufu kama Nameless alimtaka gavana Sakaja kuita barabara moja jijini Nairobi jina la E-Sir kwa  kumbukumbu za msanii huo kutokana na mchnango wa kimziki aliokuwa nao.

Nameless aliyekuwa pamoja na E-Sir wakati wa ajali iliyomwangamiza, alianza mchakato wa kukusanya sahihi katika mtandao na kufanikiwa kupata maelfu ya sahihi wakati huo na sasa ombi lake linaonekana kutimia baada ya hotuba ya gavana Sakaja kwenye sherehe za Jamhuri Dei Disemba 12, 2024.

E-Sir aliyejulikana kwa jina lake halisi kama Issah Mmari alifariki tarehe 16 Machi 2003 kwenye ajali ya barabarani akielekea Nairobi baada ya kutumbuiza mashabiki kwenye tamasha lililofanyika katika sehemu moja ya burudani jijini Nakuru. 

Baadhi ya ngoma zake zilizotamba ni pamoja na ‘Leo ni Leo’ na ‘Moss Moss’ ambazo bado zinazidi kutamba miaka kadhaa baada ya kifo chake.



 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved