logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wewe na Mama mmeunganishwa Mbinguni!" Esther Musila amkumbuka marehemu baba yake

Babake Esther Musila alikuwa na umri wa takriban miaka 73 alipofariki mwaka wa 2012.

image
na Samuel Mainajournalist

Burudani14 December 2024 - 11:51

Muhtasari


  •  Esther alisema kwamba baba yake alikufa siku kama hiyo miaka kumi na mbili iliyopita na akataka roho yake iendelee kupumzika kwa amani.
  • Miaka michache baadaye, mke huyo wa Guardian Angel alibaki kuwa yatima kwani kwa bahati mbaya mamake pia aliaga dunia.


Mke wa mwimbaji Guardian Angel Esther Musila amemsherehekea marehemu babake huku akioadhimisha miaka kumi na miwili tangu mzazi huyo wake afariki.

Katika taarifa yake ya Jumamosi, Esther alisema kwamba baba yake alikufa siku kama hiyo miaka kumi na mbili iliyopita na akataka roho yake iendelee kupumzika kwa amani.

 Pia alimtaka marehemu babake awe na amani kwani anaamini aliungana na mama yao mbinguni.

“Baba, leo unatimiza miaka 12 tangu uende kuwa na Bwana. Endelea kupumzika kwa amani kwani tunajua wewe na mama mmeungana mbinguni,” Esther alisema.

Aliambatanisha taarifa yake na picha ya kumbukumbu ya marehemu baba yake.

Babake Esther Musila alipoteza maisha mnamo Desemba 2012. Alikuwa na umri wa miaka 73 alipofariki.

Miaka michache baadaye, mke huyo wa Guardian Angel alibaki kuwa yatima kwani kwa bahati mbaya mamake pia aliaga dunia.

Mwaka jana, Bi Musila alimkumbuka marehemu mamake takriban miaka saba baada ya kuaga dunia.

Wakati akimsherehekea mzazi huyo wake, Bi Musila alimtaja marehemu kama nguzo kuu ya maisha yake.

"Ulinifundisha kuthamini kila siku ya maisha yangu na kuishi kana kwamba hakuna kesho. Nililelewa na mwanamke mwenye nguvu na najua kila wakati ulikuwa unasimama nami," alisema kwenye mtandao wa Instagram.

Musila alimuombea mzazi huyo wake mapumziko ya amani na kueleza jinsi anavyojivunia miaka ambayo walishiriki pamoja.

Hata hivyo, alieleza anavyotamani marehemu angekuwa hai ili ashuhudie maendeleo yake na akutane na mumewe Guardian Angel.

"Mama, natamani ungeishi muda mrefu zaidi ili ukutane na mwanaume mzuri zaidi katika maisha yangu sasa. Najua ungefurahi sana kuniona katika nafasi hii mpya na najua tungekuwa tukiimba nyimbo uzipendazo pamoja," alisema.

Aliongeza,"Wajukuu zako pia wamefanya upate fahari kama vile ungetaka wafanye. Endelea kutuangalia sote hadi siku moja tutakapokutana tena. Tunakukumbuka na tunakupenda milele mama."

Musila alifichua kuwa mama yake alifariki akiwa usingizini, saa chache tu baada ya yeye na kaka yake kumtembelea.

Alitaja siku ambayo mamake alifariki kama siku ya giza zaidi maishani mwake huku akisimulia matukio yaliyofuata.

"Miaka 7 iliyopita, asubuhi kama hii, nilipokea simu kwamba mama yangu mpendwa amefariki usingizini. Hii ilikuwa chini ya saa 12 baada ya mimi na kaka yangu Fred kwenda kijijini kwa wikendi. Ilikuwa siku mbaya zaidi katika maisha yetu." 

"Bado sijui tulipataje nguvu ya kuendesha gari hadi Machakos, kwa kweli ilionekana kama ndoto. Ninaamini kabisa hadi leo kwamba Mwenyezi alilisuluhisha kwa njia yake mwenyewe na alitaka tutumie saa za mwisho za maisha ya mama pamoja naye," alisema.

Esther Musila alizaliwa Machakos yapata miaka 54 iliyopita na yeye ndiye mtoto wa kwanza kuzaliwa na binti pekee wa wazazi wake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved