KENNEDY RAPUDO, mume tajiri wa mwanasosholaiti Amber Ray kwa mara nyingine tena amekanusha madai ya kuhusishwa na biashara haramu ya kutakatisha fedha na kughushi dhahabu.
Kupitia kwa taarifa ndefu kwenye ukurasa wake wa
Instagram, Rapudo alisisiti9za kwamba biasara ya kutakatisha fedha na kuuza
dhahabu bandia sio njia yake na wala haitokuja kutokea kuwa biashara yake.
Rapudo ambaye ni tajiri msiri kuhusu chanzo cha
utajiri wake alisema kwamba wachache ambao wanamfahamu vizuri wanaweza toa
ithibati kuwa utajiri wake ni halali.
“Utapeli
wa dhahabu? Utakatisaji wa fedha? Hizo sio njia zangu na haziwezi kuwa njia
zangu. Ukweli ni kwamba watu ambao wananijua kiukweli wanaelewa maadili na
kanuni zangu. Sijawai jihusisha katika kitu chochote haramu,”
Rapudo alithibitisha.
Rapudo alisema kuwa kama wale wanaofuatilia Habari za
biashara hizo haramu wanataka kupata ukweli, basi wanaweza pata majibu kutoka
kwa idara husika kama vile DCI.
Tajiri huyo alisema kwamba kwa vile aliamua kuweka
maisha yake faraghani na kuficha vyanzo vya utajiri wake haimaanishi kwamba ni
haramu.
“Kwa
vile mtu aliamua kuishi maisha ya faragha na kutanika vyanzo vya utajiri wake
haina maana kwamba wanajihusisha katika biashara haramu. Inasikitisha sana
kuona jinsi watu wameamua kujikita katika kufuatilia mambo ya watu badala ya
kuzingatia maisha yao.”
“Wakati
wanaongea, nitaendelea kusonga mbele, kujenga maisha yangu kwa njia sahihi,
njia moja ya kweli kwa kila hatua,” Rapudo aliongeza.
Rapudo alisema kuwa wakati alikuwa maskini miaka ya
nyuma, hakuna ata mtu mmoja aliyefanya uthubutu wa kufuatilia chanzo cha
utajiri wake, lakini sasa kwa vile anavyo, kila mtu yuko na uchu wa kutaka
kujua.
“Hata
hivyo, wakati nilikuwa maskini miaka ya nyuma, hakuna aliyethubutu kufuatilia
chanzo cha umaskini wangu. Ama tuseme ni wivu, njaa na roho chafu?”
alihoji.
Alisema kwamba kila mtu kwa sasa anafaa kuelekeza
nguvu zake kwa kukosoa uongozi mbaya wa serikali na si katika kupoteza usingizi
kwa utajiri wa mtu binafsi.