logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Otile Adokeza Kuchukua Likizo Kutoka Mtandaoni Kutokana Na Huzuni Kuhusu Nchi

"Huku nje ni kugumu, nyinyi [viongozi] hamwezi kuelewa hisia ya mtu asiye na chochote cha kujivunia hata baada ya kufanya kila kitu kizuri masomoni,” Otile Brown

image
na MOSES SAGWE

Burudani06 January 2025 - 13:00

Muhtasari


  • Alijiunga na vijana wengine mitandaoni ambao wamekuwa wakishinikiza kutaka kujua waliko baadhi ya vijana wanaharakati ambao waliripotiwa kutoweka baada ya ku8tekwa nyara wiki 2 zilizopita.
  • Hata hivyo, baadhi ya vijana hao wameripotiwa kuachiliwa na kuungana na familia zao mapema Jumatatu asubuhi.



MSANII wa kizazi kipya wa humu nchini Otile Brown amedokeza uwezekano wake kuchukua likizo kutoka katika mitandao ya kijamii mwaka huu.


Kupitia Instagram, Otile Brown alifichua kwamba kila wakati anapoingia katika mitandao ya kijamii, anajawa huzuni mwingi kutokana na jinsi mambo ya kisiasa yanavyotendeka.


Msanii uyo ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa katika mstari wa mbele kuikashifu serikali kutokana na kukithiri kwa visa vya utekaji nyara wa vijana kadhaa alisema kwamba kila wakati anapata huzuni mwingi kwa sababu ya nchi yake – Kenya.


Brown alisema kwamba kutokana na hilo, huenda akatatmini kuchukua likizo ya muda kutoka kwa mitandao, akisema kwamba roo yake iko huru hata kama mwili wake utachukuliwa.


“Nina huzuni kila dakika nyingine kwa sababu ya nchi yangu. Siwezi kujizuia, nadhani ninafaa kukaa nje ya mitandao ya kijamii kwa dakika moja. Chukua mwili wangu lakini roho yangu iko huru,” Otile Brown aliandika.


Kauli yake inajiri wiki moja tu baada ya kutoa kauli nyingine ya kuonya serikali dhidi ya kuendelea kuwapuuza vijana na matakwa yao.


Brown alisema kwamba imekuwa kama kawaida kwa viongozi kuona vijana kama watoto wa kuchezea shere, lakini akaonya kuwa upo wakati vijana watasema imetosha na kuamua kuchukua sheria mikononi.


“Viongozi wetu kuchochewa na vijana kwenye mitandao ya kijamii ni jambo la kushangaza sana. Unatarajia nini ukikataa kuwawezesha? Utafika wakati hawatakuwa na chochote ca kupoteza. Huku nje ni kugumu, nyinyi [viongozi] hamwezi kuelewa hisia ya mtu asiye na chochote cha kujivunia hata baada ya kufanya kila kitu kizuri masomoni,” Otile Brown alisema Desemba 28 kupitia instagram.


Alijiunga na vijana wengine mitandaoni ambao wamekuwa wakishinikiza kutaka kujua waliko baadhi ya vijana wanaharakati ambao waliripotiwa kutoweka baada ya ku8tekwa nyara wiki 2 zilizopita.


Hata hivyo, baadhi ya vijana hao wameripotiwa kuachiliwa na kuungana na familia zao mapema Jumatatu asubuhi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved