logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilienda Tz Kutafuta Harmonize Tufanye Kolabo Sababu Alipenda Ngoma Yangu – Simple Boy

“Tanzania nilikuwa nimeenda kutafuta Harmonize na Simba (Diamond Platnumz). Kwa bahati mbaya sikukutana na wao kwa sababu muda wetu na wao haukuoana."

image
na MOSES SAGWEjournalist

Burudani09 January 2025 - 14:19

Muhtasari


  • Hivyo alifunga safari kufuatilia kama angeweza kufanikisha kolabo hiyo, jambo ambalo alisema kwa bahati mbaya halikufaulu.
  • Msanii huyo aliyesafiri na meneja wake Machabe alisema kwamba alikuwa anafuatilia ahadi ya kolabo na moja kati ya wasanii wanaofanya vizuri kutoka nchini humo, Harmonize.



RAPA STEVO Simple Boy amefunguka kwa undani kiini cha ziara yake ya takribani wiki moja nchini Tanzania mwishoni mwa mwaka jana.


Akizungumza kwenye mahojiano na mwanablogu Trudy Kitui, Stevo Simple Boy alifichua kwamba ziara yake haikuwa ya kujivinjari bali ilikuwa ya kufuatilia miadi ya kikazi.


Msanii huyo aliyesafiri na meneja wake Machabe alisema kwamba alikuwa anafuatilia ahadi ya kolabo na moja kati ya wasanii wanaofanya vizuri kutoka nchini humo, Harmonize.


Alisema kwamba alihisi Harmonize alivutiwa na ngoma yake ya ‘Inauma lakini itabidi umezoea’ aliyoifanya miaka ya nyumba baada ya kumuona bosi huyo wa lebo ya Konde Music Worldwide akiimba kipande chake.


Hivyo alifunga safari kufuatilia kama angeweza kufanikisha kolabo hiyo, jambo ambalo alisema kwa bahati mbaya halikufaulu.


“Tanzania nilikuwa nimeenda kutafuta Harmonize na Simba (Diamond Platnumz). Kwa bahati mbaya sikukutana na wao kwa sababu muda wetu na wao haukuoana. Lengo langu lilikuwa, kama naweza kurudisha nyumba kitambo kidogo, kuna wakati ile ngoma yangu ‘inauma but itabidi tuzoee’ Harmonize aliimba kipande kifupi…”


“…na wakati alikuwa hapa Kenya akapigia simu meneja wangu wa kitambo akisema angetaka kufanya kazi na mimi. Lakini vitu havikuenda sawa, hivyo nilikuwa nimeenda kumtafuta huko angalau tufanye hata kolabo moja. Kwa bahati mbaya hatukuweza kukutana lakini huu mwaka nafikiri itatimia,” Stevo alieleza.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved