CHIEF GODLOVE Mwakibete, kijana mdogo mwenye utajiri wa kushangaza kutoka nchini Tanzania ameibuka na mapya akiwajibu mbona mara nyingi huwa hasafiri nje ya nchi.
Kijana huyo ambaye ameibukia kuwa gumzo kubwa
mitandaoni miezi ya hivi karibuni kutokana na utajiri wake, alisema kwamba
amekuwa akipata maswali mengi kutoka kwa watu wanaohoji mbona huwa hasafiri
kwenda kula bata katika mataifa na miji ya kitajiri kama vile Dubai na Marekani
kama matajiri wenzake.
Akijibu swali hilo kwa utani, Godlove alisema kwamba
hawezi kusafiri kuenda Dubai na Marekani kujivinjari kama matajiri wenzake, kwa
vile hakuna mtu atakayeachia nyoka wake kumlisha.
“Mnaouliza
mbona siendi Dubai na Marekani, nyoka mtalisha nyinyi? Kwendeni zenu, siendi
Marekani wala Dubai, majini yangu na mizimu atalisha nani?”
Godlove alijibu kwa utani usio wa kawaida.
Hata hivyo, kijana huyo alifuta chapisho hilo baadae
kutoka kwenye kurasa zake za Instagram na X alikokuwa amezichapisha siku ya
Alhamisi.
Jibu hilo, japo lilikuwa la kitani, lakini
lilionekana kuzua maswali mengi kuliko majibu miongoni mwa watu anaowatia moyo
katika safari ya kutafuta utajiri.
Hii si mara ya kwanza kwa mkwasi huyo mchanga kutoa
kauli za kutatanisha kuhusu Imani yake katika utajiri na Uuungu.
Siku chache zilizopita, Godlove alionekana kutilia
shaka uwepo wa mbinguni, akisema kwamba viongozi wa kidini wanaotangaza Habari za
mbinguni hata wao wenyewe hawaijui.
“Ukitaka
Habari za kwenda mbinguni hata anaekusisimulia Habari za huko ajawahi kwenda
fuatilia wachungaji na mashekhe ukitaka kujitambua wewe ninani umezaliwa
kufanya nini ili ufanikiwe Kua na uwezo wa kujitibu na kujiombea nisikilize kisha
fuata nnachokuelekeza mimi,” Godlove aliandika
kwenye X, Januari 3.
Mwaka 2025 ulipoanza, Chief Godlove alisema kwamba
ombi lake kuu mwaka huu ni Mungu kumwepushia wanawake wasiopenda hela kwani
watamfanya kuwa mzembe wa kuzitafuta.
“Mwaka 2025 mungu niepushie wanawake wasiopenda pesa
watanifanya niwe maskini,” aliomba.
Katika
