Drake ameondoa ombi la kisheria alilowasilisha dhidi ya lebo
yake, Universal Music Group (UMG) na Spotify kuhusu wimbo uliovunja rekodi wa
Kendrick Lamar ‘Not Like Us.
Nyota huyo wa Canada alichukua hatua Novemba mwaka jana, akidai kuwa kampuni hizo za muziki zilitumia bots, payola na mbinu nyingine kutangaza wimbo wa Lamar ikiwa ni pamoja na kutumia tabia isiyo halali ya kulipa kituo cha redio cha kibiashara kucheza wimbo bila kituo hicho kufichua malipo hayo, ambao ulimshutumu kuwa paedophilia.
Mwimbaji huyo alishutumu kampuni hizo kushirikiana kupunguza viwango vya leseni za utiririshaji kwenye diss track ya Kendrick.
‘’Uenezaji wa ngoma hiyo iliyovunja rekodi ‘’Not like us’’ kwenye utiririshaji , mauzo na uchezaji wa redio ulifanywa kimakusudi na unaonekana kutegemea mazoea ya kibiashara yasiyo ya kawaida na yasiyofaa,’’ Hii ni kutokana na ujumbe ulioandikiwa mahakama.
Wasimamizi wa Kampuni hiyo ya UMG walisema katika ujumbe wao kuwa pendekezo kwamba UMG itafanya chochote kudhalilisha na kupaka tope msanii wake yeyote ni ya kukera na sio kweli.
‘’Pendekezo kwamba UMG itafanya chochote kudunisha msanii wake yeyote ni jambo la kukera na si kweli na kuongeza, Tunatumia kanuni za maadili ya hali ya juu katika kampeni zetu za uuzaji na utangazaji. Hakuna kiasi cha hoja za kisheria za kubuni na za kipuuzi katika uwasilishaji huu wa kabla ya hatua unaweza inaficha ukweli kwamba mashabiki wanachagua muziki wanaotaka kusikia."
Siku ya Jumanne, mawakili wa Drake kwa hiari yao waliondoa kesi ya awali dhidi ya UMG na Spotify, na hivyo kumaliza kesi hiyo.
Hati za mahakama ya New York zilizoonwa na Rolling Stone zilisoma kuwa ‘’mlalamishi anaacha kesi hii maaalum kwa hiari kwa wajibu wote bila gharama kwa upande wowote’’
Hapo awali Drake aliwasilisha ombi lingine huko Texas, akidai UMG ililipa kundi la redio la iHeartRadio kucheza 'Not Like Us', na kwamba UMG iliruhusu kuachiliwa kwa wimbo huo licha ya kujua kuwa ulikuwa na tuhuma za Drake kuwa "certified paedophile." Ombi hili linabaki kuwa amilifu.
Wimbo huo wa ‘Not Like Us ' ilikuwa pigo la mwisho katika mzozo wa muda mrefu kati ya Drake na Lamar, wimbo ambao ulihitimisha vita vyao vya kufoka. Walakini, maoni ya umma yamegeuka zaidi dhidi ya Drake tangu wakati huo.
Baadhi ya wachambuzi wa mambo wameeleza kuwa kesi hiyo ya kisheria ilikuwa na nguvu kwa Drake kujiondoa kwenye dili lake na Universal, lakini ukweli unabaki pale pale kwamba hakuna aliyewahi kushindwa kwenye vita vya kufoka vibaya hivi na kushitakiwa hapo awali.