logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Sina Haja Kuolewa Na Diamond, Sijamshikia Bastola Anioe!” Zuchu Aipasha Wasafi

Zuchu alitishia kuwapeleka Wasafi mahakamani ikiwa wataendelea kumchokonoa kisa uhusiano wake na bosi wao, Diamond Platnumz.

image
na MOSES SAGWE

Burudani16 January 2025 - 11:59

Muhtasari


  • Lokole katika swali lake alimtaja Zuchu kama king’ang’anizi anayelazimisha kuolewa na Diamond wakati Diamond mwenyewe anakaa kama hataki vile.
  • “Kama mnaona ni rahisi sana kumng’ang’ania ambieni hao mnaotaka awe nao wakamng’ang’anie tuone.”
  • Mrembo huyo wa malkia wa taarab aliwashauri watangazaji wa Wasafi kuweka mipaka baina ya kazi yao na mambo yake akisema kwamba hawammudu hata kidogo.



MSANII kutoka lebo ya WCB Wasafi Zuchu ameamua kujibu mipigo baada ya baadhi ya wandani kutoka kwa himaya ya Wasafi kuhoji ikiwa bosi wake, Diamond Platnumz ana nia ya dhati ya kufunga ndoa naye.


Ifahamike kwamba kwa zaidi ya miaka 3 sasa, Diamond na Zuchu wamekuwa wakijidai kuwa mtu na mpenzi wake, licha ya awali kujulikana kama msanii na bosi wake.


Zuchu aliamua kufungulia mirija yake ya hasira kwa watangazaji wa Wasafi ambao walikuwa wanajadili redioni kuhusu uwezekano wa Diamond kumuoa Zuchu hatimaye.


Zogo zima lilianza pale Juma Lokole, mtangazaji katika kipindi cha Mashamsham alimuuliza Ricardo Momo, kaka wa Diamond kama kweli Diamond anaweza kumuoa Zuchu.


Lokole katika swali lake alimtaja Zuchu kama king’ang’anizi anayelazimisha kuolewa na Diamond wakati Diamond mwenyewe anakaa kama hataki vile.


Jambo hili lilionekana kumkera Zuchu ambaye kupitia Instagram alitoa pofu zito kwa Wasafi akisema kwamba yeye hana haja ya kuolewa na Diamond na wala hajawahi mshikia bunduki kumtaka ndoa.


“Hebu naomba nitoe tamko, sina haja wala silazimishi mimi kuolewa na Nasibu (Diamond). Ifike hatua mtafute vingine vya kuhoji. [Diamond] hana lazima hata ya kuwa na mimi na sijawahi kumshikia bastola wala kumteka,” Zuchu alifoka.



“Ana haki ya kwenda kokote anakoridhika. Maana naona mmeacha kazi mnafanya na sasa kazi yenu mpya ni kunichafulia chini na kutafuta commwents na likes,” mrembo huyo aliongeza kwa hasira.


Zuchu aliendelea kubwabwaja katika kile alichokitaja kama barua ya wazi kwa watangazaji hao akisema kuwa wamekuwa wakitafuta tu namna yak umuongelelea hata wakati hajafanya lolote la kuzungumziwa.


“Maana naona huyo Nasibu akiwa na mwanamke dunia nzima inaacha kazi na kuanza kumuandama. Watu wote, taasisi nzima  kipindi na vipindi vyote ikitokea siku hata mtu iwe birthday yake mnatafutatu namna mniongelelee,” alisema.


Alimalizia kwa kuwaambia ikiwa wanaona kumng’ang’ania Diamond ni rahisi kama wanavyosema anamng’ang’ania, basi wako huru kumtafuta mwanamke wanayetaka wamlete amng’ang’anie Diamond.


“Kama mnaona ni rahisi sana kumng’ang’ania ambieni hao mnaotaka awe nao wakamng’ang’anie tuone.”



Mrembo huyo wa malkia wa taarab aliwashauri watangazaji wa Wasafi kuweka mipaka baina ya kazi yao na mambo yake akisema kwamba hawammudu hata kidogo.


Zuchu alitishia kuwapeleka Wasafi mahakamani ikiwa wataendelea kumchokonoa kisa uhusiano wake na bosi wao, Diamond Platnumz.


“Mshauri [Diaomond] aniache muone kama nitamfuata na mabomu. Wajinga nyinyi hebu choreeni mipaka, sio kutwa kujifanya mnanimudu. Sasa nasubiri nione, safari hii nitapeleka mtu mahakamani,” alimaliza.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved