logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Khadija Kopa, Mamake Zuchu Adokeza Diamond Hatamuoa Bintiye!

"Hayo ni mambo ya kawaida tu, ikifika siku ataolewa. Na mimi sijasema DIAMOND, nimesema muda ukifika Mungu akimjaalia atapata mume atamuoa,” mama Kopa alisema.

image
na MOSES SAGWE

Burudani20 January 2025 - 11:04

Muhtasari




KHADIJA Kopa, mamake msanii kutoka WCB Wasafi, Zuchu amekuwa mtu wa hivi punde kutia neno kuhusu zogo linaloendelea baina ya mwanawe na chombo cha Habari cha Wasafi FM lakini pia na bosi wake Diamond Platnumz.


 Kopa alizungumza na waandishi wa Habari wakati wa mkutano wa chama tawala Tanzania, CCM ambapo aliweka wazi kwamba mwanawe Zuchu muda ukifika atapata tu mwanamume sahihi wa kumuoa.


Hii ni baada ya Diamond kuonekana akikana kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Zuchu kwenye kipindi cha Netflix, licha ya kudai kuwa mpenzi wake kwa miaka 3 sasa.


Khadija Kopa alisema kwamba hajasema kama Diamond atamuoa mwanawe na kusisitiza kuwa Zuchu bado hajachelewa kupata mpenzi sahihi wa kufunga ndoa naye.


“Haditih za sijui mwanangu aolewi hazinikwazi kwa sababu sio mimi ndio naolewa. Pia sio mimi ndio niliyemwambia mtu muoe. Hayo ni mambo ya kawaida tu, ikifika siku ataolewa. Na mimi sijasema DIAMOND, nimesema muda ukifika Mungu akimjaalia atapata mume atamuoa,” mama Kopa alisema.


Kopa alitaja sekeseke za Diamond na Zuchu kama upuzi ambao hana muda wa kushughulika nao.


“Mimi sishughuliki na upuzi wao, mimi nashughulika na mambo yangu tu. Hayo mambo hata msiniulize,” Khadija Kopa alisema.


Kauli hizi zinajiri siku chache tu baada ya Diamond kuonekana kumdhalilisha Zuchu kwa kumkana bayana kwenye tamthilia ya Young, Famous & African iliyotoka mwishoni mwa juma lililopita.


Hata hivyo, Diamond kwenye mitandao ya kijamii aliwataka mashabiki kuacha kumfitinisha na Zuchu akijitetea kwamba ule ni mchezo tu kwenye tamthilia na wala si kila kitu alichokiigiza pale kinamaanisha ukweli katika maisha yake ya uhalisia na Zuchu.


Msanii huyo alisema kwamba anambeza sana Zuchu na kuonyesha kwamba bado anampenda licha ya kuwa tofauti kwenye Netflix.


Zuchu na mtangazaji wa Wasafi, Juma Lokole wiki jana walizua mtafaruku mkali kwenye Instagram, baada ya Lokole kumtaja kuwa king’ang’anizi anayelazimisha ndoa kwa Diamond.


Kauli hiyo ilimkera Zuchu ambaye alifuta utambulisho wa WCB Wasafi kwenye bio yake Instagram na hata kutishia kuivuta lebo hiyo mahakamani kwa kudai kwamba ananyanyazwa.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved